WANAOWANIA TUZO 13 LIGI KUU YA VODACOM


Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania limetangaza wanamichezo wote wanaowania tuzo 13 kwenye hafla ya washindi wa Ligi Kuu ya Vodacom kwa msimu wa 2015/2016 itakayofanyika Jumapili (Julai 17 mwaka huu) kwenye hoteli ya Double Tree by Hilton jijini Dar es Salaam.
Aina 13 za tuzo ya Ligi hiyo inayodhaminiwa na kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania zitatolewa kwa washindi chini ya uratibu wa Kamati ya Tuzo ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) inayoundwa na waandishi wa habari za michezo, makocha, viongozi (administrators) na wawakilishi kutoka kwa wadhamini (Vodacom na Azam Tv).
Tuzo hizo na kiasi cha fedha wanazopata washindi kwenye mabano ni
  1. Bingwa (sh. 81,345,723) 
  2. Makamu bingwa (sh. 40,672,861)
3. Mshindi wa tatu (sh. 29,052,044)
4. Mshindi wa nne (sh. 23,241,635)
 5. Timu yenye Nidhamu Bora (sh. 17,228,820)
*Zilizopendekezwa kuwania tuzo hiyo ni:
– JKT Ruvu
– Mgambo Shooting na
– Mtibwa Sugar
6. Mchezaji Bora wa Ligi (sh. 9,228,820)
*Waliopendekezwa (nominees) kuwania tuzo hiyo ni:
– Shiza Kichuya (Mtibwa Sugar)
– Juma Abdul (Yanga) na
– Mohamed Hussein (Simba)
7. Mfungaji bora (sh. 5,742,940)
8. Kipa Bora (sh. 5,742,940)
*Waliopendekezwa (nominees) kuwania tuzo hiyo ni:
– Aishi Manula (Azam),
– Beno Kakolanya (Tanzania Prisons) na
– Deogratius Munishi (Yanga)
9. Mchezaji Bora wa Kigeni (sh. 5,742,940)
– Donald Ngoma (Yanga)
– Thabani Kamusoko (Yanga)
– Vincent Agban (Simba)
10.  Kocha Bora (sh. 8,000,000)
*Waliopendekezwa (nominees) kuwania tuzo hiyo ni:
– Hans Van Pluijm (Yanga)
– Mecky Maxime (Mtibwa Sugar) na
– Salum Mayanga (Tanzania Prisons)
11.  Mwamuzi bora (sh. 5,742,940)
*Waliopendekezwa (nominees) kuwania tuzo hiyo ni:
– Anthony Kayombo
– Ngole Mwangole
– Rajab Mrope
12. Mchezaji Bora Chipukizi (sh. 4,000,000
*Waliopendekezwa (nominees) kuwania tuzo hiyo ni:
– Farid Mussa (Azam)
– Mohamed Hussein (Simba)
– Mzamiru Yasin (Mtibwa Sugar) na
– Shiza Kichuya (Mtibwa Sugar)
13. Goli bora la msimu (sh. 3,000,000)
  1. *Kinyang’anyiro cha goli bora ni:
    – Ibrahim Ajib (magoli mawili ) na
– Amisi Tambwe  (goli moja)

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*