Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (wa pili kulia) akitoa maelekezo kwa Meneja wa Kiwanja cha ndege cha Kikwetu Mkoani Lindi Bw. Boniface Njanda (Wa kwanza Kulia) wakati alipotembelea uwanja huo.
Meneja wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) mkoa wa Lindi Eng. Isaac Mwanawima akitoa taarifa ya utendaji wa Wakala huo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (wa kwanza kushoto) wakati alipotembelea wakala huo.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa Meneja wa Wakala wa Majengo (TBA) mkoa wa Lindi Eng. Hillary Msaki, wakati alipotembelea wakala huo,mkoani Lindi.
Mtaalam wa ufundi na Mitambo wa Kampuni ya Simu nchini (TTCL) akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa namna ya Mitando ya TTCL inavyofanya kazi, Mkoani Lindi.
Comments