Edward Lowassa akipata maelezo mbalimbali kutoka viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama kutoka napolisi kuuzuia kikao cha ndani cha Mh.Edward Lowassa na wanachama wa Chadema wa wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya ambacho kilizuiwa kufanyika na Jeshi la Polisi asubuhi ya leo.
Sehemu ya askari polisi wakiwa kwenye eneo ambalo lilitegemewa kufanyika kikao cha ndani cha Mh.Edward Lowassa na wanachama wa Chadema wa wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya ambacho kilizuiwa kufanyika na Jeshi la Polisi asubuhi ya leo.
Edward Lowassa akiondoka na msafara wake baada ya kupata maelezo mbalimbali kutoka viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama kuzuiwa kufanyika kwa kikao cha ndani cha Mh.Edward Lowassa na wanachama wa Chadema wa wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya ambacho kilizuiwa kufanyika na Jeshi la Polisi asubuhi ya leo.
Baadhi ya Wananchi wakitazama tukio hilo
--
Lowassa ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema alianzia ziara yake mkoani hapa tangu Agosti 21 na juzi alifanya vikao vya ndani katika majimbo yanayoshikiliwa na wabunge wa chama chake mkoani Songwe wakati leo asubuhi alitarajiwa kwenda Katavi na Rukwa.
Katika Mikoa ya Rukwa na Katavi alitarajiwa kufanya mikutano ya ndani Majimbo ya Nkasi Kaskazini na Kusini na Sumbawanga.
Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini wanayoiita ‘Kanda ya Nyasa’, Frank Mwaisumbe alisema kwamba polisi walimpigia simu Lowassa juzi saa 1.00 jioni akiwa Tunduma wakimtaka aahirishe ziara yake Mkoa wa Rukwa.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Rukwa, Gorge Kyando alipoulizwa kwa njia ya simu alisema waliwashauri viongozi wa Chadema wapange siku nyingine ya ziara kwa sababu mkoa ulikuwa na ugeni mkubwa.
Comments