Wiki moja
kabla ya Ligi Kuu England kuanza huwa ni kawaida kuchezwa mchezo wa
ngao ya jamii, mchezo ambao huzikutanisha timu Bingwa wa Ligi Kuu na
Bingwa wa Kombe la FA, August 7 2016 England katika uwanja wa Wembley
Leicester City ambaye ni Bingwa wa EPL na Man United ambaye ni bingwa wa
FA.
Huo
ulikuwa mchezo wa kwanza wa mashindano kwa kocha Jose Mourinho
aliyejiunga na Man United msimu huu sambamba na nyota Zlatan Ibrahimovic
aliyetumia mechi hiyo kudhihirisha ubora wake wa kucheka na nyavu,
katika mchezo huo Man United wamefanikiwa kuibuka na ushindi wa goli
2-1.
Man
United ndio walikuwa wa kwanza kupata goli dakika ya 31 kupitia kwa
Jesse Lingard ila Leicester City walisawazisha goli hilo dakika ya 52
kupitia kwa mshambuliaji wao aliyeng’ara msimu uliopita Jarmie Vardy
lakini furaha ya Leicester City ilimalizwa na Zlatan Ibrahimovic dakika
ya 83 na kuipa Man United ubingwa wa Ngao ya Hisani
Comments