RAIS MAGUFULI APIGA MARUFUKU WAMACHINGA KUONDOLEWA


Rais John Magufuli amepiga marufuku operesheni za kuwaondoa mijini wamachinga badala yake ameziagiza mamlaka husika kuboresha mazingira ya biashara kwa kundi hilo.
“Hakuna kuondoa machinga mjini kwani huko nje mnakowapeleka hakuna wateja,” ilikuwa ni kauli ya Rais Magufuli iliyopokewa kwa shangwe na umati wa wakazi wa Mwanza uliofanyika katika Viwanja vya Furahisha.
Amesema kila mtu ana haki ya kuishi mjini na kuendesha shughuli halali za kiuchumi zitakazomwezesha kuwa na maisha bora kulingana na sheria, kanuni na taratibu, hivyo ni wajibu wa halmashauri za majiji, manispaa, miji na wilaya kuwawezesha wamachinga kuendesha shughuli zao.


“Viongozi wa mikoa wakae na kujadiliana nao (wamachinga) kuona ni sehemu gani watawapeleka kwa kuzingatia mazingira mazuri ya kufanya biashara,” ameagiza.

Hata hivyo, Rais Magufuli aliwaonya wamachinga kuhusu tabia ya kukubali kutumiwa na wafanyabiashara wakubwa kwa kuwauzia bidhaa zao na hivyo kuikosesha mapato Serikali.

Rais Magufuli amerejea agizo lake kwa halmashauri zote nchini na mamlaka nyingine zinazohusiana na ukusanyaji wa kodi kuacha kuwarundikia kodi na ushuru wa kero wakulima na wajasiriamali wadogo, badala yake, nguvu nyingi zielekezwe kwenye kukusanya kodi kutoka kwa wafanyabiashara wakubwa.

“Ninataka kodi, lakini siyo kwa watu maskini wakiwemo wakulima na wajasiriamali wadogo, bali kwa wafanyabiashara wakubwa. Machinga ndiyo walionichagua, hivyo sitaki wabughudhiwe. Hatuwezi kuwa na Serikali nzuri tukiwasumbua wananchi.”amesema

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*