Na Dotto Mwaibale
UONGOZI wa Shule za Feza nchini umeibuka na kukanusha taarifa zilizozagaa kwenye mitandao ya kijamii, kuwa wao hawana uhusiano na Fethullah Gulen wala serikali ya Uturuki kwa vile hawajawahi kupokea misaada toka pande hizo mbili za uendeshaji na kuwa shule hizo hazitafungwa.
Kauli hiyo imetolewa baada ya hivi karibuni kuenea kwa uvumi kuwa shule za Feza zipo hatarini kufungwa kwa madai kuwa mmiliki wake ni yule aliyejihusisha na jaribio la kuipindua serikani nchini Uturuki.
Mwenyekiti wa Bodi wa Shule hizo, Habibu Miradji aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na wanahabari Kawe jijini Dar es Salaam leo asubuhi.
Alisema Watanzania wanapaswa kufahamu kuwa Shule za Feza ni kama
Comments