SIMBA SC WAREJEA DAR, WAINGIA KAMBINI NDEGE BEACH

Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
SIMBA SC imehamisha kambi yake kutoka Morogoro hadi Dar es Salaam leo.
Simba SC imeingia kambini Dege Beach Hotel, Dar es Salaam leo ikitokea Chuo cha Biblia mjini Morogoro.  
Kikosi kimelazimika kuwahi Dar es Salaam kwa ajili ya kuazimisha wiki ya Simba kuelekea kielele cha sherehe za miaka 80 ya klabu, maarufu kama Simba Day Jumatatu ijayo.
Na Simba SC imekuja mjini siku moja baada ya kufungwa 1-0 na KMC ya Kinondoni jioni ya Jumatano katika mchezo wa kirafiki uliofanyika Uwanja wa Highlands, Bigwa mkoani Morogoro.
Kikosi cha Simba kilichofungwa 1-0 na KMC jana

Huo ulikuwa mchezo wa kwanza Simba SC kupoteza chini ya kocha mpya, Mcameroon, Joseph Marius Omog baada ya awali kushinda mechi zote tatu, 5-0 dhidi ya Burkina Fasso, 2-0 dhidi ya Moro Kids na 6-0 dhidi ya Polisi Morogoro.
Katika kilele cha sherehe za Simba Day, Wekundu wa hao Msimbazi watamenyana na AFC Leopards ya Kenya iliyochukua nafasi ya Interclube ya Angola ambayo imejitoa dakika za mwishoni.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.