UFUNGUZI WA MAFUNZO KUHUSU MWONGOZO WA USIMAMIZI WA UWEKEZAJI WA UMMA KWA MIKOA YA TABORA, KIGOMA, SHINYANGA NA KATAVI
Mgeni Rasmi Bibi. Florence Mwanri,
Kaimu Katibu Mtendaji, Tume ya Mipango (aliyesimama) akitoa hotuba ya ufunguzi
wa mafunzo kuhusu Mwongozo wa Usimamizi wa Uwekezaji wa Umma kwa Maofisa na watendaji wa Idara za Sera na Mipango
kutoka mikoa ya Tabora, Kigoma, Shinyanga na Katavi. Wengine ni Bi. Lorah
Madete, Kaimu Naibu Katibu Mtendaji, Klasta ya Uchumi Jumla, Tume ya Mipango
(kushoto) na Dr. Jehovaness Aikaeli, Mhadhiri Mwandamizi na Mkuu wa Idara ya
Uchumi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Washiriki wa Mafunzo kuhusu Mwongozo wa Usimamizi wa
Uwekezaji wa Umma ambao ni Maofisa
na Watendaji wa Idara za Sera na Mipango kutoka mikoa ya Tabora, Kigoma,
Shinyanga na Katavi wakimsikiliza kwa makini Mgeni Rasmi (hayupo pichani)
wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo yanayofanyika Mkoani Tabora.
Bi. Lorah Madete, Kaimu Naibu
Katibu Mtendaji, Klasta ya Uchumi Jumla, Tume ya Mipango, akitoa neno kwa
Maofisa na watendaji wa Idara za Sera na Mipango kutoka mikoa ya Tabora,
Kigoma, Shinyanga na Katavi ambao ni washiriki wa mafunzo yanayohusu Mwongozo wa Usimamizi wa
Uwekezaji wa Umma kabla ya
kumkaribisha mgeni rasmi ili afungue mafunzo hayo ya siku tano. Waliokaa ni Bibi. Florence Mwanri, Kaimu
Katibu Mtendaji, Tume ya Mipango (katikati) na Dr. Jehovaness Aikaeli, Mhadhiri
Mwandamizi na Mkuu wa Idara ya Uchumi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Washiriki wa mafunzo kuhusu Mwongozo wa Usimamizi wa Uwekezaji wa Umma kwa Maofisa na watendaji wa Idara za Sera na Mipango kutoka mikoa ya Tabora, Kigoma, Shinyanga na Katavi pamoja na wawezeshaji wa mafunzo wakiwa katika picha ya pamoja na Mgeni Rasmi Bibi. Florence Mwanri, Kaimu Katibu Mtendaji, Tume ya Mipango (aliyekaa katikati) mara baada ya ufunguzi wa mafunzo hayo.(PICHA NA THOMUS NYIMBO-TUME YA MIPANGO)
Comments