WAZIRI WA AFYA AITAKA MOI KUHUDUMIA WAGONJWA KWA HARAKA ZAIDI.

moi1Waziri wa  Afya ,Maendeleo ya jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wa pili kushoto akitoa maagizokwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) Dkt. Samuel Swai  wa kwanza kulia wakati alipotembelea  wagonjwa katika hospitali hiyo leo jijini Dar es salaam.
moi2Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) Dkt. Samuel Swai  wa kwanza kulia akifafanua jambo kwa Waziri wa  Afya ,Maendeleo ya jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikati alipotembelea  wagonjwa katika hospitali hiyo leo jijini Dar es salaam
moi3Waziri wa  Afya ,Maendeleo ya jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiwajulia hali baadhi ya wagonjwa waliopo katika taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI)alipotembelea  wagonjwa katika hospitali hiyo leo jijini Dar es salaam.
moi4
Waziri wa  Afya ,Maendeleo ya jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikati akimfariji mtoto Rahel Razaro wa kwanza kushoto aliyelazwa katika Taasisi ya Mifupa Muhimbili(MOI) alipotembelea  wagonjwa katika hospitali hiyo leo jijini Dar es salaam na wa kwanza kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Taasisi hiyo Dkt. Samuel Swai.
……………………………………………………………………………………………………………..
Na Ally Daud-Maelezo
Serikali chini ya Wizara ya Afya ,Maendeleo ya jamii, Jinsia , Wazee na Watoto imeitaka Taasisi ya Mifupa Muhimbili(MOI) kuhudumia wagonjwa haraka iwezekanavyo ili kuondoa msongamano wa wagonjwa hospitalini hapo na kuwaruhusu wakaendelee na shughuli za kujenga taifa.
Akizungumza hayo alipotembelea wagonjwa  MOI Waziri wa  Afya ,Maendeleo ya jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu aliwataka watumishi wa taasisi hiyo kuwahudumia wagonjwa haraka iwezekanavyo ili kuwapa fursa ya kwenda kufanya shughuli za kimaendeleo kwa ajili ya taifa.
“Mnatakiwa kuhudumia wagonjwa kwa haraka na ufanisi mkubwa ili kuwasaidia watanzania kutotumia muda mwingi wakiwa hospitalina na badala yake wapone waende wakaendelee na shughuli zao za kujenga taifa kwa maendeleo ya Nchi yetu”alisema Mhe. Ummy
Aidha Mhe. Ummy ameongeza kuwa licha ya kuwa na changamoto zinazojitokeza hospitalini hapo Wizara ipo bega kwa began a Taasisi hiyo  kuhakikisha huduma bora zinatolewa kwa wananchi chini ya kitengo hiko ili kufikia malengo ya milenia.
“Nafahamu kama kuna changamoto zinazoikabili taasisi hii kama mlivyonieleza lakini tupo pamoja katika kuziondoa na nyinyi hakikisheni mnafanya kazi kwa bidii ili kuondoa  malalamiko ya wananchi na kuleta huduma bora na kwa wakati” alisisitiza Mhe. Ummy.
Mbali na hayo Mhe. Ummy ameitaka taasisi hiyo kurudisha huduma ya kufanya upasuaji kwa wagonjwa siku za jumamosi bila ya kukosa tena kwa haraka ili kupunguza mlundikano wa wagonjwa kwenye taasisi hiyo.
Kwa upande wa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji MOI Dkt. Samuel Swai amesema kuwa wamepokea agizo hilo na wapo tayari kufanya kazi kwa bidii ili kuokoa maisha ya watanzania kwa haraka na ubora zaidi.
“Tupo tayari kutekeleza agizo la Mheshimiwa Waziri la kufanya kazi kwa bidii ili kuokoa maisha ya watanzania kwa haraka na ataona matokeo mazuri kuanzia leo hii” alisisitiza Dkt. Swai.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*