KILI QUEENS YAWAFUMUA 3-2 RWANDA NA KUTINGA NUSU FAINALI YA CHALLENGE JINJA


Na Mwandishi Wetu, JINJA
TIMU ya taifa ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Queens imefuzu Nusu Fainali ya michuano ya Kombe la Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge kufuatia ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Rwanda leo Jinja, Uganda.
Kwa kuwa Kundi B lina timu tatu, nyinginr Ethiopia – ushindi wa leo unaihakikishia Kili Queens tiketi ya Nusu Fainali.   
Mabao ya Kili Queens inayofundishwa na Sebastian Nkoma, yamefungwa na Asha Rashid ‘Mwalala’ dakika za 11 na 65 na Stumai Abdallah dakika ya 28, wakati ya Rwanda yamefungwa na Ibangarrue Marie na Amina Ally wa Tanzania Bara aliyejifunga.
Kikosi cha Kilimanjaro Queens kilichoshinda 3-2 dhidi ya Rwanda leo mjini Jinja, Uganda

Kili Queens watashuka tena dimbani kumenyana na Ethiopia Septemba 16, mwaka huu katika mchezo wa mwisho wa kundi lake. Rwanda na Ethiopia zitakamilisha mechi za Kundi B kwa kumenyanaa na Septemba 14.
Nusu Fainali zitafuatia Septemba 18, kabla ya fainali kufanyika Septemba 20, 2016 ikitanguliwa na mchezo wa kusaka mshindi wa tatu.
Mchezaji wa Kili Queens akifumua shuti leo Jinja dhidi ya Rwanda
Mchezaji wa Kili Queens akimiliki mpira mbele ya wacheaji wa Rwanda leo Jinja


Manahodha wa Tanzania Bara (kushoto) Sofia Mwasikili na wa Rwanda (kulia)

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.