Mtengenezaji wa Sauti katika chaneli ya
StarTimes Kiswahili, Tracy Luo (katikatio) akizungumza na waandishi wa
habari (hawapo pichani) wakati wa kutangaza kufanyika kwa fainali za
shindano la vipaji vya sauti litakalofanyika kesho katika ukumbi wa
Nkrumah, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Kushoto ni mshiriki wa shindano
hilo kutoka Zanzibar, Safiya Ahmed na kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa
Masoko wa kampuni hiyo, Damien Li. Washiriki 18 kati ya 547 wameingia
hatua ya fainali ambapo washindi 10 watajipatia fursa ya kwenda kufanya
kazi makao makuu ya StarTimes yaliyopo Beijing, China.
Mshiriki Safiya Ahmed kutoka Zanzibar (kushoto), akizungumza katika mkutano huo. Kulia ni Mtengenezaji wa Sauti katika chaneli ya StarTimes Kiswahili, Tracy Luo.
Comments