YANGA YAZINDUKA, YAITANDIKA MAJIMAJI 3-0, TAMBWE AANZA FUJO ZA MABAO LIGI KUU

Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
YANGA SC imezinduka katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baada ya kuichapa Maji Maji ya Songea mabao 3-0 jioni ya leo Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Mfungaji bora wa Ligi Kuu msimu uliopita, Amissi Joselyn Tambwe alifunga mabao mawili kipindi cha pili baada ya kiungo Deus David Kaseke kutangulia kufunga kipindi cha kwanza.
Yanga sasa inafikisha pointi saba, baada ya kucheza mecni tatu, ikishinda mbili na sare moja – sawa na mahasimu wao, Simba SC.
Winga Simon Msuva hakuwa mwenye bahati leo, baada ya kupoteza nafasi kadhaa za kufunga mabao, ikiwemo penalti. 
Msuva alipiga penalti mbili zote akafunga, lakini refa akamuamuru kurudia, ya kwanza akidaiwa kutishia kabla ya kupiga na ya pili, refa akisema wachezaji wenzake walisogea kabla hajapiga.
Amissi Tambwe (katikati) akipongezwa na wenzake baada ya kufunga bao la tatu leo
Msuva alipokwenda kupiga kwa mara yatatu, mpira ukagonga mwamba na kurudi uwanjani kabla ya kutokea piga nikupige na kumkuta Kaseka aliyefunga dakika ya 19.
Tambwe akaifungia Yanga bao la pili kwa kichwa akimalizia pasi ya Simon Msuva kufuatia krosi ya Juma Mahadhi. Tambwe akafunga bao la tatu akimalizia krosi ya Mahadhi tena.
Mechi nyingine za Ligi Kuu leo, Mwadui FC imelazimishwa sare ya 2-2 na ndugu zao Stand United Uwanja wa Mwadui Complex, Shinyanga, Mbeya City imefungwa nyumbani 2-1 na Azam FC na Ndanda FC imelazimishwa sare ya 0-0 na Kagera Sugar, Ruvu Shooting imewalza ndugu zao JKT Ruvu 1-0 Uwanja wa Mabatini, Mlandizi Pwani. 
Kikosi cha Yanga kilikuwa; Ally Mustapha ‘Barthez’, Juma Abdul, Mwinyi Hajji, Vincent Andrew/Kevin Yondan dk85, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Thabani Kamusoko, Simon Msuva/Yussuf Mhilu dk88, Obrey Chirwa/Juma Mahadhi dk46, Amissi Tambwe, Donald Ngoma na Deus Kaseke. 
Maji Maji: Agathon Anthony, Bahati Yussuf, Suleiman Kibuta, Hamad Kibopile, Ernest Raphael, Lulanga Mapunda, Alex Kondo, Mfanyeje Yusuph, Hassan Hamisi, Marcel Bonivanture na Paul Mahona/Peter Mapunda dk55.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI