ZANZIBAR LEO IMEPIGWA 9-0 TU NA UGANDA

Na Mwandishi Wetu, JINJA
ZANZIBAR imepoteza mchezo wake wa pili katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati (CECAFA Challenge) baada ya kufungwa mabao 9-0 na wenyeji Uganda leo mjini Jinja.
Zanzibar iliyofungwa 10-1 na Burundi katika mchezo wa kwanza wa Kundi A, sasa itakamilsha mechi zake za kundi hilo kwa kumenyana na Kenya keshokutwa wakati imekwishaaga mashindano hayo.
Tanzania Bara, Kilimanjaro Queens keshokutwa inacheza mechi yake ya mwisho ya Kundi B dhidi ya Ethiopia mjini Jinja.
Uganda wameifunga Zanzibar 9-0 leo mjini Jinja
Kilimanjaro Queens itahitaji ushindi Ijumaa ili tu kuongoza Kundi B na kupata mpinzani tahfifu kidogo katika Nusu Fainali.
Hiyo inatokana na kwamba, Kilimanjaro Queens juzi ilijihakikishia kufuzu Nusu Fainali ya michuano hiyo baada ya ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Rwanda.
Mabao ya Kili Queens inayofundishwa na Sebastian Nkoma, yalifungwa na Asha Rashid ‘Mwalala’ dakika za 11 na 65 na Stumai Abdallah dakika ya 28, wakati ya Rwanda yamefungwa na Ibangarrue Marie na Amina Ally wa Tanzania Bara aliyejifunga.  Rwanda na Ethiopia zitakamilisha mechi za Kundi B kwa kumenyanaa na leo.
Nusu Fainali zitafuatia Septemba 18, kabla ya fainali kufanyika Septemba 20, 2016 ikitanguliwa na mchezo wa kusaka mshindi wa tatu.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.