Rais Dkt John Pombe Magufuli akikagua pembe za ndovu 50 zilizokamatwa katika operesheni maalum ya kusaka majangili alipofanya ziara ya kushtukiza makao makuu ya Wizara ya Maliasili na Utalii (MPINGO HOUSE) jijini Dar es salaam leo Oktoba 29, 2016
Rais Dkt John Pombe Magufuli akimpongeza kwa kazi nzuri Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi baada ya kukagua akikagua pembe za ndovu 50 zilizokamatwa katika operesheni maalum ya ya kusaka majangili alipofanya ziara ya kushtukiza makao makuu ya Wizara ya Maliasili na Utalii (MPINGO HOUSE) jijini Dar es salaam leo Oktoba 29, 2016o
Rais Dkt John Pombe Magufuli akimpongeza kwa kazi nzuri Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi baada ya kukagua akikagua pembe za ndovu 50 zilizokamatwa katika operesheni maalum ya ya kusaka majangili alipofanya ziara ya kushtukiza makao makuu ya Wizara ya Maliasili na Utalii (MPINGO HOUSE) jijini Dar es salaam leo Oktoba 29, 2016o
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU
Simu:
255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Faksi: 255-22-2113425
|
OFISI
YA RAIS,
IKULU,
1 BARABARA YA BARACK OBAMA,
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 29 Oktoba,
2016 amefanya ziara ya kushtukiza katika Ofisi za Wizara ya Maliasili na Utalii
(Mpingo House) kwa lengo la
kufuatilia utekelezaji wa operesheni ya kukabiliana na ujangili inayofanywa na
Kikosi Kazi kilichoundwa na Wizara hiyo.
Akiwa
katika ofisi hizo Rais Magufuli aliyekuwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili
na Utalii Meja Jenerali Gaudensi Milanzi ameshuhudia pembe 50 za ndovu zilizokamatwa
kati ya jana Ijumaa na leo Jumamosi Jijini Dar es Salaam.
Aidha,
Dkt. Magufuli ameoneshwa magari yaliyokamatwa yakiwa yamebeba pembe hizo na watuhumiwa
wanane wanaodaiwa kujihusisha na mtandao wa biashara haramu ya pembe za ndovu.
Rais
Magufuli amewapongeza askari wote waliopo katika Kikosi Kazi cha kudhibiti na
kupambana na biashara haramu ya pembe za ndovu pamoja na Raia wema wote
wanaotoa ushirikiano katika operesheni hiyo na amewahakikishia kuwa anatambua
kazi kubwa wanayoifanya na anawaunga mkono.
“Nawapongeza
sana kwa kazi nzuri mnayoifanya na ninawahakikishia kuwa ninawaunga mkono,
chapeni kazi, wakamateni wote wanaojihusisha na biashara hii haramu, hakuna wa
kumbakiza, awe mkubwa au nani, kamateni, wala msijali cheo chake, umri wake,
dini yake, kabila lake, umaarufu wake, sheria ni msumeno, watafuteni wote mpaka
watu wakiona tembo wawe wanakimbia wenyewe ili tuokoe wanyama wetu ambao
wanaendelea kutekelezwa.
“Hapa
mmekamata pembe 50 maana yake tembo 25 wameuwawa, haiwezekani maliasili yetu
ikawa inapotea hovyo hovyo kwa sababu ya watu wachache wenye tamaa ya kutaka
utajiri wa haraka haraka” amesisitiza Rais
Magufuli.
Gerson
Msigwa
Mkurugenzi
wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar
es Salaam
2
Comments