kampuni mpya ya Bima ya Clarckson Yazinduliwa jijini Dar, TPSF yakaribisha ubunifu zaidi kwenye sekta ya hiyo nchini



2b
Mgeni Rasmi katika uzinduzi wa Kampuni ya Clarkson Insurance Brokers inayojishughulisha na masuala ya bima Bw. Godfrey Simbeye ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF akionyesha zawadi aliyokabidhiwa na Mwenyekiti wa Kampuni ya Clarkson Insurance Brokers Justin Lambert mara baada ya uzinduzi wa kampuni hiyo uliofanyika kwenye hoteli ya Hyyat Kilimanjaro Kempinski jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki.
cl9
Mgeni Rasmi katika uzinduzi wa Kampuni ya Clarkson Insurance Brokers inayojishughulisha na masuala ya bima Bw. Godfrey Simbeye ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF akizungumza wakati alipozindua Kampuni ya bima ya Clarkson Insurance Brokers kwenye hoteli ya Hyyat Kilimanjaro Kempinski jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki.
cl01
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Parkal Randall ambayo ni Kampuni Tanzu ya Clarkson Insurance Brokers Bw. Coutts Otolo akizungumza kwenye uzinduzi wa kampuni ya Clarkson Insurance Brokers inayojishughulisha na masuala ya bima, katika uzinduzi uliofanyika mwishoni mwa wiki kwenye hoteli ya Hyyat Kilimanjaro Kempinski jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki
cl1
Jaji Mkuu wa Tanzania Mh. Mohamed Othman Chande akisalimiana na Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Biashara wa Kampuni ya JUNACO Group Of Companies Limited ambayo ni Mwanahisa Mzawa Bw. Anic Kashasha wakati wa uzinduzi wa Kampuni ya Bima ya Clarckson Insurance Brokers jijini Dar es salaam.
cl002
Mwenyekiti wa Kampuni ya Clarkson Insurance Brokers Justin Lambert akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampuni hiyo uliofanyika kwenye hoteli ya Hyyat Kilimanjaro Kempinski jijini Dar es salaam.
cl10
Meneja Mkuu wa Kampuni hiyo Tanzania Bw.Patrick Marimo akifafanua jambo kwa waandishi wa habari .
3b
Jaji Mkuu wa Tanzania Mh. Mohamed Chande Othman akizungumza na Balozi Mstaafu Peter Kalaghe wakati wa uzinduzi wa kampuni ya Clarkson Insurance Brokers inayojishughulisha na masuala ya bima katika uzinduzi uliofanyika mwishoni mwa wiki kwenye hoteli ya Hyyat Kilimanjaro Kempinski jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Parkal Randall ambayo ni Kampuni Tanzu ya Clarkson Insurance Brokers Bw. Coutts Otolo.
4b
Jaji Mkuu wa Tanzania Mh. Mohamed Chande Othman akimsikiliza Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Parkal Randall ambayo ni Kampuni Tanzu ya Clarkson Insurance Brokers Bw. Coutts Otolo wakati walipokuwa wakibadilishana mawazo kwenye uzinduzi wa kampuni ya Clarkson Insurance Brokers inayojishughulisha na masuala ya bima, katika uzinduzi uliofanyika mwishoni mwa wiki kwenye hoteli ya Hyyat Kilimanjaro Kempinski jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki
cl1
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Parkal Randall ambayo ni Kampuni Tanzu ya Clarkson Insurance Brokers Bw. Coutts Otolo wa tano kutoka kulia na Justin Lambert Mwenyekiti wa Kampuni ya Clarkson wakikata keki kuashiria uzinduzi wa kampuni hiyo katika ofisi yao iliyopoghorofa ya nane jengo la IPS Mtaa wa Samora jijini Dar es salaam kabla ya uzinduzi rasmi.
cl2
Baadhi ya wafanyakazi wakiwa katika picha ya pamoja.
cl3 cl02
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Parkal Randall ambayo ni Kampuni Tanzu ya Clarkson Insurance Brokers Bw. Coutts Otolo akiwatambulisha watendaji wa mbalimbali wa kampuni hiyo.
cl2
wageni waalikwa mbalimbali pamoja na wafanya kazi wa kampuni hiyo wakiwa katika uzinduzi huo.
cl3 cl5 cl6
Mwanamuziki John Muhina kulia akiimba pamoja na wanamuziki wenzake wa bendi ya Tanzanite Band katika uzinduzi huo.
cl7
Wageni waalikwa mbalimbali wakiwa katika uzinduzi huo.
cl8
..................................................................
Na Mwandishi wetu,
Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) imekaribisha uwekezaji zaidi kwenye sekta ya Bima nchini ili kuibua ushindani utakaochochea ubunifu wenye tija zaidi kwa wadau wa sekta hiyo.
Akizungumza mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa kampuni mpya ya Bima ijulikanayo kama Clarkson Insurance Brokers Tanzania Limited,Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF , Bw. Godfrey Simbeye alisema ustawi wa uchumi wa nchi kwa sasa unahitaji uimara na ubunifu zaidi kwenye sekta ya bima hivyo wingi wa kampuni hizo unaweza kuwa na tija zaidi katika kufanikisha hilo.
“Tanzania kwa sasa ipo kwenye utekelezaji wa miradi mikubwa kama ile ya bomba la mafuta, ujenzi wa reli ya kati, ujenzi wa barabara na majengo makubwa ya kisasa, vyote hivi vinahitaji kulindwa na bima hivyo ujio wa kampuni kama hii ya Clarkson Insurance Brokers Tanzania Limited tunauona kama ni heri na wenye tija kwa taifa,’’ alibainisha.
Kwa mujibu wa Bw Simbeye kwa sasa mchango wa sekta ya Bima kwenye Ukuaji wa Pato la Taifa (GDP) ni chini ya asilimia 1 huku akiitaja sekta binafsi kuwa ni miongoni mwa sekta ambazo bado hazijafaidi ipasavyo matunda ya uwepo wa huduma za Bima ambapo alitaja suala la ukosefu wa ubunifu miongoni mwa makampuni ya Bima kuwa ni moja ya sababu ya uwepo wa changamoto hiyo.
“Matumaini yangu kwa kampuni ya Clarkson Insurance Brokers Tanzania Limited kwa kiasi kikubwa yanachochewa na ukongwe wao wa miaka 58 wakitoa huduma hii nchini Kenya ikiwa ni pamija na Uganda hivyo natarajia kwamba uzoefu wao katika kipindi hicho kirefu unaweza kuwa na tija zaidi hapa nchini,’’ aliongeza.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa makampuni ya Bima ya Clarkson Insurance Brokers Tanzania Group Bw Justin Lambert alisema pamoja na kutoa huduma kwa weledi, kampuni yake itajikita zaidi katika kutoa elimu ya bima kwa jamii ili kuwavutia zaidi wengi ambao kwasasa bado hawajaingia kwenye huduma hiyo.
“Clarkson Insurance Brokers hatujaingia hapa nchini ili kuongeza idadi ya makampuni ya bima yaliyopo nchini bali lengo letu hasa kuongeza ushindani na kuleta mapinduzi makubwa na yenye tija kwa wadau wa sekta hii muhimu,’’ alibainisha.
Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo hapa nchini Bw, Patrick Marimo alisema mafanikio ya kampuni hiyo katika soko lake jipya hapa nchini kwa kiasi kikubwa yatachochewa na ubunifu mkubwa wa kampuni hiyo katika utoaji wa huduma zake.
“Tunalenga kuleta mabadiliko makubwa kwenye huduma hii muhimu na ndio maana pamoja na mambo mengine tutajikita zaidi katika kutoa elimu kwa jamii ili kuijengea uelewa zaidi kwenye masuala ya bima ili tutoe huduma kwa watu wenye uelewa zaidi …lakini pia uwekazaji wetu kwenye teknolojia ya kisasa unaweza kuwa chachu zaidi katika kufikia malengo,’’ alisema.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI

KOCHA WA AL.AHLY ASEMA YANGA NI TIMU BORA NA NGUMU