Mahafali ya kidato cha nne Sullivan Provost yafana.


 Mkurugenzi Mtendaji wa Shule ya Wavulana ya Sullivan Provost,  Rachel Mwalukasa (kushoto), akizungumza wakati wa  mahafali ya pili ya kidato cha nne ya shule hiyo shuleni hapo, Kibaha kwa Mathias mkoani  Pwani hivi karibuni. Wengine kutoka  kulia ni Mkuu wa Shule, Alex Nicholaus, Mhadhiri kutoka  Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,  Dk Ellen Kilinga na Mhandisi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ya UDSM (COICT), Dk Suzan Lujara aliyekuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo. 
 Mhandisi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ya UDSM (COICT), Dk Suzan Lujara (wa pili kulia) akimpongeza Mohamed Ibrahim, mmoja wa wanafunzi waliofanya vizuri kimasomo na kujizolea kutwaa tuzo mbalimbali wakati wa mahafali ya pili ya kidato cha nne ya shule hiyo shuleni hapo, Kibaha kwa Mathias, Pwa
​n​i hivi karibuni. Wengine kutoka Kulia ni Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM, Dk Ellen Kilinga, Mkurugenzi Mtendaji was Sullivan Provost, Rachel Mwalukasa na Mkuu wa shule hiyo, Alex Nicholaus.  
 Mhandisi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (COICT), Dk Suzan Lujara (wa pili kulia) akikabidhi cheti kwa Alvin Mgaya, mmoja wa wahitimu wa kidato cha nne wa Shule ya Sekondari ya wavulana ya Sullivan Provost wakati wa mahafali ya pili ya shule hiyo, shuleni hapo  Kibaha kwa Mathias, Pwani hivi karibuni. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa shule hiyo, Rachel Mwalukasa na Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dk. Ellen Kilinga.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Shule ya Sekondari ya Wavulana ya Sullivan Provost,  Rachel Mwalukasa (katikati), akimlisha keki mmoja wa wahitimu wa kidato cha nne wa shule hiyo wakati wa mahafali yao ya pili shuleni hapo, Kibaha kwa Mathias, Pwani hivi karibuni.
 Wahitimu wa kidato cha nne wa Shule ya Sekondari ya Wavulana ya Sullivan Provost wakipozi katiaa picha ya kumbukumbu pamoja nja baadhi ya walimu, viongozi wa shule na mgeni rasmi wakati wa  mahafali yao shuleni hapo, Kihaba, Pwani.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shule ya Wavulana ya Sullivan Provost,  Rachel Mwalukasa (katikati), akimpongeza Mkuu wa shule hiyo Alex Nicholaus  katika mahafali ya pili ya kidato cha nne ya shule hiyo shuleni hapo, Kibaha kwa Mathias, Pwani hivi karibuni. Anayeangalia ni mmoja wa wajumbe wa kamati ya wazazi wa shule hiyo, Janeth Alexander.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI