MOI WAFANIKIWA UPASUAJI WA MKUBWA WA KIBIONGO

Taassisi ya MOI imefanikiwa kufanya upasuaji wakunyoosha mfupa wa mgongo wa mtoto hivi karibuni uliopinda (Kibiongo) kitaalamu (Scoliosis).  kupitia madaktari bingwa wa MOI walioko kwenye mafunzo ya ubobezi wa juu katika upasuaji wa mifupa na mgongo kwa watoto  kwa kushirikiana na madaktari bingwa kutoka Marekani(PICHA NA MAKTABA MOI)
10/12/2016, Dar es Salaam, Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) kwa mara ya kwanza imefanya upasuaji mkubwa kwa mafanikio makubwa wa kunyoosha mfupa wa mgongo wa mtoto uliopinda (Kibiongo) kitaalamu (Scoliosis).
Upasuaji huo umefanyika kwa kutumia technolojia ijulikanayo kama ‘Posterior Instrumentation and Fusion’ ambayo inahusisha uwekaji wa vyuma maalum kwenye mfupa wa mgongo uliopinda katika sehemu ya juu na chini ya mfupa wa mgongo  na kuufanya mgongo unyooke kama inavyotakiwa
Taassisi ya MOI imefanikiwa kufanya upasuaji huo  kupitia madaktari bingwa wa MOI walioko kwenye mafunzo ya ubobezi wa juu katika upasuaji wa mifupa na mgongo kwa watoto  kwa kushirikiana na madaktari bingwa kutoka Marekani
Aidha, Uanzishwaji wa upasuaji huu umetokana na kuanzishwa kwa ushirikiano wa kimafunzo kati ya Taasisi ya MOI na Chuo cha madaktari bingwa wa upasuaji cha Afrika Mashariki , Kati na Kusini ‘COSECSA’ na Madaktari bingwa kutoka Marekani
Uanzishwaji wa upasuaji huu wa kunyoosha migongo ya watoto iliyopinda (Scoliosis) unatarajiwa kuisaidia serikali kupunguza rufaa za kuwapeleka wagonjwa nje ya nchi ambazo ni za gharama kubwa. Ambapo gharama za kumtibu mtoto mmoja nje ya nchi ni zaidi ya dola za kimarekani elfu 30 hadi 40
Hivyo, Uongozi wa Taasisi ya MOI unatoa wito kwa madaktari kwote nchini kuja kupata mafunzo hayo hapa MOI, Pia wazazi wenye watoto wenye matatizo hayo wawalete hospitali ili wafanyiwe uchunguzi na upasuaji
-xxxx-
Imetolewa na,


Patrick J. Mvungi

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.