SERIKALI YAPIGA MARUFUKU UPIGAJI PICHA WODINI


MANISPAA ya Songea Mkoa wa Ruvuma kuanzia sasa imepiga  marufuku vitendo vya upigaji picha wodini kwa kutumia kamera au simu za mkononi katika hospitali na vituo vyake vyote vya afya.
Manispaa ya Songea inatekeleza agizo la Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma ambalo ni agizo  la Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto ambalo linaeleza kuwa kumekuwa na tabia ya wananchi kupiga picha wodini wanapofika kuwajulia hali ndugu zao ambapo baadhi ya picha wanazopiga zimekuwa zinaoneshwa kwenye mitandao ya kijamii zikiwa na  ujumbe wenye kupotosha jamii.Hata hivyo wakurugenzi wanatakiwa kuwaelimisha wananchi umuhimu wa kuwasilisha malalamiko yao inapotokea ukiukwaji wowote katika utoaji huduma za afya.
Na Albano Midelo Songea

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.