WAZIRI DK. POSSI: UELEMAVU NA UZEE SIO LAANA



Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Watu wenye Walemavu Dkt. Abdallah Possi akiongea na wageni waalikwa hawapo pichani wakati wa uzinduzi wa taarifa mpya ya utafiti inayobainisha hali halisi ya ulemevu na uzee nchini jijini Dar es salaam.

……………………………………………………..

Na Eleuteri Mangi, MAELEZO

Watafiti wa masuala mbalimbali ya kijamii nchini wametakiwa kuhakikisha wanafanya tafiti ambazo zitawasaidia watu wenye ulemavu kupata vifaa saidizi ili waweze kumudu kuendesha maisha yao ya kila siku.

Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Watu wenye Walemavu Dkt. Possi Abdallah alipokuwa akizindua taarifa mpya ya utafiti inayobainisha hali halisi ya ulemevu na uzee nchini jijini Dar es salaam.

“Serikali inafarijika inapoona watu wanafanya utafiti ili kuwasaidia watu wenye ulemavu waweze kupata vifaa saidizi na ni kitu gani kifanyike ili NGOs ziweze kujikwamua kiuchumi na kuwasaidia wenye mahitaji” alisema Dkt. Possi.

Kuhusu suala la unyanyapaa kwa watu wenye ulemavu, Dkt. Possi amesema kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu hapo tayari kuona wananchi wananyanyapaliwa huku akisisitiza kuwa watu wote ni sawa na ofisi hiyo ina “zero tolerance” kwa watu wanaowanyayapaa mlemavu.

Katika masuala ya kisheria kwa watu wenye ulemavu, Dkt. Possi amesema kuwa inapotokea mlemavu au mzee amefanyiwa kosa taarifa itolewe mara moja ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya waliofanya makosa hayo na haki iweze kutendeka.

Naibu Waziri Dkt. Possi pia amezitaka Asasi zinazoshughulika na watu walemavu wafanye kazi kwa pamoja ili kuwasaidia walengwa ambao ni walemavu, watoto na wazee na kuwataka kutumia fursa waliyonayo ya kupata msaada kisheria bure kutoka kwenye taasisi za sheria ikiwemo Chama cha Mawakili (Tanganyika Law Society), TAMWA pamoja na taasisi nyingine za kisheria wakati masuala ya jianai amewataka wayapeleke kwenye polisi kwa hatua zaidi za kisheria huku akisisitiza kumshirikisha inapobidi kufanya hivyo.

Akitoa maelezo ya utafiti huo wakati wa uzinduzi, mtafiti kutoka Taasisi ya Afya Ifakara (IHI) Bakar Fakih amesema kuwa utafiti huo umewashirikisha watafiti rika mbalimbali wakiwemo wazee na watu wenye ulemavu na kubainisha kuwa bado kuna imani potofu kwenye jamii juu ya wazee na watu wenye ulemavu.

Utafiti huo unaoongozwa na kaulimbiu “Ulemavu na uzee sio laana” umebainisha kuwa watu wenye ulemavu na wazee nchini wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo kupata elimu, huduma za afya, unayanyasaji wa kingono na kuvunjika kwa ndoa, kutokujaliwa na familia pamoja na kutengwa kwa watu wenye ualbino kutokana na mila potofu.

Kwa upande wake mtafiti rika Blandina Isaya amesema kuwa walemavu waachwe wafanye maamuzi yanayohusu maisha yao ikiwemo masuala ya ndoa wawe huru kuchagua wenza wao badala ya kuchaguliwa na familia zao kwa kuwa wanahaki kama watu wengine wasio na ulemavu.

Katika kuhakikisha familia zinakuwa imara kiuchumi, Blandina amesema kuwa familia zenye watu wenye ulemavu na wazee wapewe elimu ya ujasiriamali ili waweze kuwa na uwezo wa kuendesha maisha yao kwa kulea familia ipasavyo na kuomba Seriklai za mtaa ziwe na takwimu za wazee na watu wenye ulemavu.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA