AZAM FC WATAKA KUMSAJILI KABUNDA WA MWADUI FC


Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
AZAM FC inataka kuboresha zaidi kikosi chake kwa kumsajili winga wa Mwadui FC ya Shinyanga, Hassan Kabunda.
Na tayari Mwadui wameshitukia mpango huo na leo wametoa onyo kwa timu ya Alhaj Sheikh Said Salim Awadh Bakhresa na familia yake. 
Kocha wa Mwadui FC, Khalid Adam ameiambia BIN ZUBEIRY SPORTS – ONLINE leo kwamba Azam FC wanapaswa kufuata taratibu kama wanamtaka Kabuda.
Hassan Kabunda (kulia) yupo kwenye rada za Azam FC, timu inayomilikiwa na bilionea Alhaj Sheikh Said Salim Awadh Bakhresa na familia yake 

“⁠⁠Kabunda bado ana mkataba na Mwadui. Hivyo kama Azam wanamtaka, wake kuzungumza na sisi, huo ndiyo utaratibu,”amesema.
Mtoto huyo wa beki wa zamani wa kimataifa wa Yanga, Salum Kabunda aliyevuma kwa majina ya utani ya Ninja na Msudan (sasa marehemu) ni kati ya wachezaji wanaofanya vizuri katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara tangu msimu uliopita.
Na mchezaji huyo wa zamani wa Ashanti United ya Ilala, Dar es Salaam mapema msimu huu alikaribia kusajiliwa na Simba SC kama si kushindwana dau.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI

KOCHA WA AL.AHLY ASEMA YANGA NI TIMU BORA NA NGUMU