Profesa Museru: Wauguzi Toeni Huduma Bora kwa Wagonjwa


Mkurugenzi  Mtendaji wa Hospitali ya Taifa  Muhimbili- MNH,  Profesa   Lawrence Museru amewataka wauguzi kufanya kazi kwa bidii  na kuzingatia maadili  ya Uuguzi ili kutoa huduma bora kwa wagonjwa wanaofika kupata huduma  katika hospitali hiyo.

Profesa Museru  ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es salaam  katika  mkutano  wa wauguzi  Tawi la Muhimbili  uliolenga kumpongeza  kwa kuteuliwa  kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali hiyo .

Profesa Museru  amesema  licha ya  wauguzi hao kukabiliwa changamoto mbalimbali  lakini hawanabudi kufanya kazi kwa bidii na kuonyesha upendo kwa wagonjwa  ili kukabiliana na ushindani na kutoa huduma  bora.

“ Hii ni hospitali ya Taifa inatoa huduma za kibingwa hivyo ni lazima huduma zitolewe kwa kiwango cha juu kulingana na hadhi yake” amesema Profesa Museru.

Akisoma Risala kwa niaba ya wauguzi  Katibu wa TANNA  Taifa  Sebastian Luziga   amesema wauguzi wa MNH  wanamshukuru Profesa Museru kwa jinsi anavyojitoa kuwasaidia katika mambo mbalimbali  na kwamba  hali hiyo inaonyesha anathamini taaluma ya uuguzi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Profesa Lawrence Museru akizungumza na wauguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili katika mkutano uliofanyika leo hospitali hapo.


Baadhi ya wauguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili wakimsikiliza kwa makini Profesa Museru katika mkutano ulioandaliwa na Chama cha Wauguzi Tawi la Muhimbili .
Mkurugenzi wa Huduma ya Uuguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Agnes Mtawa akimkabidi tuzo Profesa Museru kwa lengo la kumshukuru na kutambua mchango anaotoa kwa wauguzi wa hospitali hiyo.
Katibu wa TANNA Taifa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Tawi la TANNA MNH Sebastian Luziga akimvisha Medali Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi Agnes Mtawa kama ishara ya kumshukuru kwa malezi mazuri kwa chama hicho.
Mkurugenzi Mtendaji wa MNH Profesa Museru akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wauguzi mara baada ya kufunga mkutano huo uliofanyika mapema leo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*