Muhtasari
- Trump anakadiriwa kushinda West Virginia, Kentucky, Indiana, Tennessee, South Carolina, Oklahoma na Alabama.
- Clinton anakadiriwa kushinda Vermont, jimbo anamotoka Bernie Sanders, New Jersey, DC, Massachusetts, Maryland, Delaware, Illinois na Rhode Island
- Wapiga kura zaidi ya 45 milioni walipiga kura mapema
- Muda wa kupiga kura eneo la Durham, North Carolina umeongezwa
- George W Bush amesema hakupigia Clinton au Trump kura ya urais
Habari za moja kwa moja
Wafuasi wa wagombea wakuu wa urais nchini Marekani Hillary Clinton na Donald Trump wamepokea matokeo yanayoendelea kutangazwa kwa hisia tofauti mjini New York.
Timu ya Trump ilitaraji kwamba mgombea wao angeshinda uchaguzi kama jana lakini matokeo ya uchaguzi yamewakosoa.
Mwandishi wa BBC Chris Gibson amekuwa akizungumza na wafuasi wa Clinton katika mkutano wake huko New York,akiwemo mfuasi mmoja ambaye alidhani kwamba matokeo hayo yangemfanya 'atapike'.
Comments