TSHABALALA AJITIA PINGU SIMBA SC HADI JUNI 2018


Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
BEKI wa kimataifa wa Tanzania, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ leo amesaini mkataba mpya wa miaka miwili kuendelea kuichezea Simba SC.
Tshabalala mwenye umri wa miaka 21 sasa, amesaini leo ofisini kwa Rais wa Simba SC, Evans Elieza Aveva katikati ya Jiji la Dar es Salaam.
Na Tshabalala anaongeza mkataba Simba SC katikati ya tetesi za kutakiwa na wapinzani, Azam na Yanga. 
Beki wa Simba SC, Mohammed Hussein 'Tshabalala' (kulia) akibadilishana fomu na Rais wa klabu hiyo, Evans Aveva (kushoto) baada ya kusaini mkataba mpya wa miaka miwili leo ofisini kwa kiongozi huyo

Tshabalala (kulia) na Aveva (kushoto) wakati wa kusaini mikataba leo Dar es Salaam

Bado haijajulikana Simba SC imempa kiasi gani cha fedha Tshabalala kuongeza mkataba, lakini habari za ndani zinasema amesaini kwa Sh. Milioni 30.  
Tshabalala alisaini Simba SC Juni mwaka 2014 akitokea Kagera Sugar ya Misenyi mkoani Kagera, ambayo nayo ilimtoa Azam FC.
Aliyefanikisha usajili wake kwa mara ya kwanza ni Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe aliyekigundua kipaji hicho.
Hans Poppe akimzawadia gari aina ya Toyota Raum Tshabalala Septemba mwaka huu
Tshabalala wakati anasaini mkataba wa kwanza wa kujiunga na Simba mbele ya Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya klabu hiyo, Zacharia Hans Poppe (kulia) 

Na baada ya kazi nzuri kwa misimu yake miwili ya kwanza, Poppe alimzawadia gari aina ya Toyota Raum Septemba mwaka huu.
Mtoto huyo wa dada wa beki wa zamani wa Yanga, Said Mwaibambe Zimbwe (sasa marehemu) kwa sasa ameanza kupangwa katika kikosi cha kwanza cha Taifa Stars mbele ya beki wa Yanga, Mwinyi Hajji Mngwali.  

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI