KIKAO CHA KAMATI KUU YA CCM CHAFANYA TATHMINI YA UCHAGUZI MKUU WA 2015, MAAZIMIO KUPELEKWA NEC JUMANNE


Na Bashir Nkoromo, Dar
Kikao cha Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kilichofanyika leo chini ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk. John Magufuli, kimefanya tathimni ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba mwaka jana, na kuibuka na mambo kadhaa ambayo yatafikishwa kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa CCM (NEC) keshokutwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jioni hii, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nauye amesema, tathmini hiyo ya uchaguzi, imefanywa na Kamati Kuu ikiwa ni sehemuya utamaduni wa CCM, kufanya thathmini kila baada ya uchaguzi mkuu.

"Tathmini hizi hutusaidia sana, kujua wapi tulifanya vizuri na wapi hatukufanya vizuri na mengineyo yote yaliyokuwa sehemu ya ushiriki wa Chama katika uchaguzi mkuu, na tumekuwa tukifanya hivi katika chaguzi zote hali ambayo imeifanya CCM kuimarika zaidi", alisema Nape.

Alisema, mapendekezo au hoja zote zilizoibuliwa na wajumbe katika kikao hicho cha Kamati Kuu ya CCM zitawasilishwa katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM-NEC, ambacho kitafanyika keshokutwa, jijini Dar es Salaam.

Nape amesema, pia kwamba, kutokana na kufanyika vizuri na kwa umahiri mkubwa, Kikao cha Kamati Kuu kimemalizika leo, na hakitakuwepo kesho kama ilivyokuwa imepangwa hapo awali.
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa habari, kwenye Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam.Picha: Bashir Nkoromo

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*