Mwimbaji Ambwene Mwasongwe |
WAKATI siku za tamasha kubwa la kihistoria mjini Mafinga mkoani Iringa zimezidi kusogea ,mkuu wa jimbo la kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) jimbo la Mafinga mchungaji Antony Kipangula ndie atakayezindua tamasha hilo .
Kwaya ya vijana KKKT usharika wa Iringa mjini siku ilipotembelea bungeni Dodoma |
Akizungumza leo na mwandishi wa habari hizi ,Mratibu wa tamasha hilo Mary Mungai aliyesa kuwa uzinduzi wa tamasha hilo utakwenda sambamba na uzinduzi wa ukumbi wa kisasa KWA AJILI ya burudani na shughuli mbali mbali ukumbi wa MAM ulipo katikati ya mji wa Mafinga na kuwa washindi wa uimbaji KKKT nchini kwaya ya vijana usharika wa kanisa kuu Iringa na mwimbaji wa nyimbo za injili maarufu nchini Ambwene Mwasongwe wataongoza kupamba tamasha hilo pamoja na kwaya nyingine na waimbaji binafsi kutoka ndani na nje ya Mafinga .
" kutakuwa na waimbaji wengine mbali mbali pamoja na burudani nyingine na kuwa lengo la tamasha hilo pamoja na kutoa burudani kwa wakazi wa wilaya ya Mufindi na mikoa ya Iringa na Njombe bado itakuwa ni siku ya uzinduzi wa ukumbi wa burudani na sherehe mbali mbali katika mji huo wa Mafinga"
Mungai alisema kuwa kwa ajili ya kuwashukuru wananchi wa mji wa Mafinga kwa ushirikiano mbali mbali ambao wameendelea kuutoa amelazimika kuandaa tamasha hilo ambalo wananchi watashuhudia kwa kiingilio kidogo sana kama sehemu ya kuchangia gharama ndogo ndogo za maandalizi ya tamasha na mchango kwa V.I.P utakuwa ni Tsh 10,000 wakati kawaida kwa watu wazima ni Tsh 5000 na watoto ni Tsh 3000 pekee na kuwa ili kuepusha msongamano mlangoni tiketi tayari zinauzwa katika ofisi ya shule ya Southern Highlands Mafinga , Hazina Bima na Stationary ya Huruma Msigala na getini pia zitauzwa .
Alisema pamoja na kuwa wilaya ya Mufindi ni moja kati ya wilaya zenye uchumi mkubwa hapa nchini na watu wake ni wale wanaopenda burudani mbali mbali zikiwemo za matamasha ya nyimbo za injili ila bado kumbi nyingi zilizokuwepo haziwezi kukidhi mahitaji ya burudani na kuwa kuzinduliwa kwa ukumbi huo kutafungua milango ya uchumi kwa mji huo kwa wadau kutoka ndani ya wilaya ya Mufindi na nje ya mkoa kufika kuutumia ukumbi huo kuandaa burudani mbali mbali na hata kuutumia kwa mikutano mikubwa .
Mwenyekiti wa kwaya ya vijana usharika wa kanisa kuu Kombo Mdegella akizungumzia juu ya maandalizi ya ushiriki wao katika tamasha hilo alisema kwaya yake ambayo imekuwa ikifanya vema katika mashindano mbali mbali ya uimbaji ipo kwenye maandalizi makubwa ya kuhakikisha wanatoa burudani ya nyimbo kali kwenye Tamasha hilo .
ukumbi pekee katika mikoa ya nyanda za juu kusini kujengwa kisasa na utakuwa na majukwaa mawili moja la kati litakuwa ni jukwaa linalotembea pia kutakuwa na V.I.P kwa wageni maalum ambao ili waweze kuingia ukumbini watapandishwa ghorofani kwa ngazi maalum na kushuka kwa ngazi hadi jukwaani iwapo watataka kutoingilia mlango wa waalikwa wote .
Comments