NIYONZIMA HAYUMO KABISA KIKOSI CHA KWANZA CHA LWANDAMINA YANGA


Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
KIUNGO wa kimataifa wa Rwanda, Haruna Hakizimana Fadhil Niyonzima hayumo kabisa katika kikosi cha Yanga kinachomenyana na JKU ya Zanzibar jioni ya leo katika mchezo wa kirafiki.
Kocha Mzambia, George Lwandamina amepanga kikosi chake cha kwanza Yanga leo kwa ajili ya mchezo na timu ya Jeshi la Kujenga Uchumi na Niyonzima hayumo kabisa kwa sababu ni mgonjwa.
Haruna Niyonzima (kushoto) hayumo kabisa katika kikosi cha Yanga kinachomenyana na JKU ya Zanzibar jioni ya leo katika mchezo wa kirafiki

Lwandamina aliyechukua nafasi ya Mholanzi, Hans van der Pluijm ambaye sasa anakuwa Mkurugenzi wa Ufundi, amewapanga; Ally Mustafa 'Barthez', Hassan Kessy, Oscar Joshua, Pato Ngonyani, Nadir Haroub 'Cannavaro', Said Juma, Juma Mahadhi, Matheo Antony, Obrey Chirwa, Malimi Busungu na Geoffrey Mwashuiya.
Katika benchi Lwandamina aliyeanza kazi Yanga wiki mbili zilizopita amewaweka Deogratius Munishi 'Dida', Juma Abdul, Mwinyi Hajji Mngwali, Andrew Vincent 'Dante', Simon Msuva, Vincent Bossou, Thabani Kamusoko, Justin Zulu, Donald Ngoma, Amissi Tambwe, Deus Kaseke na Kelvin Yondani.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*