Roboti inayoweza kushiriki ngono kutengenezwa


  • 22 Disemba 2016
Roboti inayoweza kushiriki ngono na binadamu huenda ikazinduliwa mwaka ujaoImage copyrightGETTY IMAGES
Image captionRoboti inayoweza kushiriki ngono na binadamu huenda ikazinduliwa mwaka ujao
Je ungependelea kushiriki ngono na roboti? ungefunga ndoa na roboti? na Je roboti anaweza kuwa na haki ya kupinga ndoa hiyo?
Haya ni baadhi ya maswala machache yanayoulizwa katika mkutano wa pili wa kuwa na mpenzi wa roboti mbali na kushiriki naye ngono katika chuo kikuu cha Goldsmith mjini London baada ya serikali ya Malaysia ambayo ndio iliokuwa taifa la maandalizi ya mkutano huo kuupiga marufuku.
Hatua hiyo imezua utata sio tu kwa mataifa yenye maoni ya Kihafidhina .
Hakukuwepo na wawakilishi kutoka kwa sekta ya ngono wala roboti za ngono katika mkutano huo.
Ni watu wachache walioweza kusema kuwa roboti Pepe alikuwa na maumbile ya kuvutiaiImage copyrightGETTY IMAGES
Image captionNi watu wachache walioweza kusema kuwa roboti Pepe alikuwa na maumbile ya kuvutiai
Kampuni ya Real Dolls inayotengeza wanaserere wa ngono ilidai kwamba itatengeza roboti wa ngono aliye na akili bandia mwaka ujao.
Uzinduzi huo iwapo utafanyika utakuwa ushahidi wa David Levy ambaye amekuwa akitabiri ujio wa roboti zinazofanana na binadamu zenye akili bandia.
Alitoa hotuba ya kufunga mkutano huo ambapo alipendekeza utengezaji wa roboti za ngono.
''Tuna roboti za urafiki na sasa roboti ambaye anaweza kuwa mpenzi ndio mtindo mpya''.
Kwa wengine kushiriki ngono na roboti ni ndoto yao lakini kwa wengine ni uharibifu mkubwaImage copyrightGETTY IMAGES
Image captionKwa wengine kushiriki ngono na roboti ni ndoto yao lakini kwa wengine ni uharibifu mkubwa
Katika kipindi cha miaka 10 ijayo, inawezakana kutengeza roboti ambayo watu wataihitaji kama mpenzi, ina upendo, inaaminika, inaheshima na hailalamiki alisema.
Wengi watapendelea uhusiano huo wa roboti na huenda wakataka kufunga ndoa nao.
Mpango huo wa mpenzi wa aina ya roboti huenda akazua maswali kadhaa ya kimaadili, hususana wakati ambapo sheria italazimika kutambua roboti kama binaadamu.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.