WACHEZAJI YANGA WASITISHA MGOMO, WAAHIDIWA KULIPWA KABLA YA IJUMAA


Na Prince Akbar, DAR ES SALAAM
HATIMAYE wachezaji wa Yanga wamesitisha mgomo wao uliodumu kwa siku mbili, baada ya kuahidiwa kulipwa mishahara yao ya Novemba kabla ya ijumaa.
Mmoja wa wachezaji wa Yanga ameiambia Bin Zubeiry Sports – Online usiku huu kwamba wamemaliza mgomo wao baada ya kuahidiwa kwamba wataingiziwa mishahara kabla ya mechi ijayo, Ijumaa dhidi ya African Lyon.
“Tumemalizana, wametuambia kila kitu wataweka sawa na kabla ya mechi (Ijumaa) kila  mtu atakuwa amekwishaingiziwa mshahara wake,”amesema mchezaji huyo ambaye hakutaka kutajwa.
wachezaji wa Yanga wamesitisha mgomo wao uliodumu kwa siku mbili, baada ya kuahidiwa kulipwa mishahara yao ya Novemba kabla ya Ijumaa

Wachezaji wa Yanga kwa siku ya pili leo wameendelea na mgomo wa kufanya mazoezi wakishinikiza walipwe mishahara yao ya Novemba.
Ni wachezaji wawili tu walioonekana Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam asubuhi ya leo, kipa Ally Mustafa ‘Barthez’ na beki Oscar Joshua.
Zaidi ya hapo walitokea makocha tu, George Lwandamina na Wasaidizi wake, Noel Mwandila Mzambia mwenzake na wazalendo, Juma Mwambusi, kocha wa makipa Juma Pondamali, Meneja Hafidh Saleh, Daktari Edward Bavu, Mchua Misuli Jacob Onyango na Mtunza Vifaa Mohammed Omar ‘Mpogolo’.
Kaimu Katibu Mkuu wa Yanga, Baraka Deusdedit alifika Uwanja wa Uhuru na kukutana na hali hiyo ya kushangaza na akaenda kuzungumza na Lwandamina baadaye Mwambusi na Hafidh.
Baada ya hapo wote wakaondoka na leo asubuhi mazoezi hayakufanyika Yanga. 
Mgomo huo ulianza jana ghafla Uwanja wa Uhuru, wachezaji wakiwa wamekwishavaa, wakagoma kuingia mazoezini.
Mapema leo, uongozi wa Yanga ulikanusha kuwapo kwa madai ya mishahara ya Novemba na kudai kwamba wachezaji wanagoma wakitaka walipwe mapema mishahara ya mwezi huu, Desemba.
“Kinacholeta matatizo hapa ni kubadilika kwa mfumo wa ulipaji, yaani badala mwishoni mwa mwezi, sasa tunalipa mwanzoni mwa mwezi. Sasa wachezaji wanataka mishahara ya Desemba walipwe mapema kwa sababu ya hizi sikukuu,”alisema Baraka akizungumza na Bin Zubeiry Sports – Online leo. 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*