Bunge la Gambia laongeza muhula wa Jammeh



Yahya Jammeh aliingia madarakani kwa njia ya mapinduzi mwaka 1994Haki miliki ya pichaAFP
Image captionYahya Jammeh aliingia madarakani kwa njia ya mapinduzi mwaka 1994
Bunge la Gambia limeongeza muhula wa Rais wa Gambia Yahya Jammeh ambao unakamilika siku ya Alhamisi kufuatia kushindwa kwake kwenye uchaguzi kwa siku 90.
Bunge pia limeidhinisha uamuzi wa Jammeh wa kutangaza hali ya tahadhari ya siku 90, katika taifa hilo dogo la Afrika Magharibi.
Viongozi wa kanda wametishia kutumia nguvu za kijeshi kumlazimisha bwana Jammeh kuondoka madarakani, ikiwa atakataa kusalimisha mamlaka kwa rais mteule Adama Barrow.
Maelfu ya watalii raia Uingereza na Uholanzi wanaondolewa kutoka Gambia.
Nchi hiyo ni maarufu kwa watalii kutokana na fukwe zake.
Gambia ilitumbukia kwenye mzozo baada ya bwana Jammeh kukataa ushindi wa bwana Barrow kwenye uchaguzi wa tarehe mosi mwezi Disemba.
Viongozi wa kanda wameshindwa kumshawishi Bwana Jammeh kuwacha madaraka.
Nigeria imetuma meli ya kivita kumshinikiza bwana Jammeh kuondoka madarakani.
Muungano wa nchi za magharibi mwa Afrika Ecowas, umeandaa kikosi kinachoongozwa na Senegal lakini bado unasema kwa hatua za kijeshi ndizo zitakuwa za mwisho.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI