JAMHURI
YA MUUNGANO WA TANZANIA
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU
Simu:
255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Faksi: 255-22-2113425
|
OFISI YA RAIS,
IKULU,
1 BARABARA YA BARACK
OBAMA,
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA KWA UMMA
Kurugenzi
ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu inapenda kuwataarifu wananchi wote kuwa Rais wa
Jamhuri ya Muungano Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, atamuapisha Kaimu Jaji Mkuu
wa Tanzania Mhe. Jaji Prof. Ibrahim Hamis Juma leo tarehe 18 Januari, 2017
Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Tukio
la kuapishwa kwa Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania litafanyika kuanzia saa 10:00
Jioni na litarushwa moja kwa moja na vituo vya Redio na Televisheni vya Shirika
la Utangazaji Tanzania (TBC), na Tovuti rasmi ya Ikulu ambayo ni
www.ikulu.go.tz
Wananchi
wote mnaalikwa kufuatilia matangazo hayo.
Gerson
Msigwa
Mkurugenzi
wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu
Dar
es Salaam
Comments