Marekani: Ilikuwa ajabu Urusi kuingilia uchaguzi wa 2016



Urusi inalalamikiwa kudukua taarifa za uchaguzi wa Marekani 2016
Image captionUrusi inalalamikiwa kudukua taarifa za uchaguzi wa Marekani 2016
Mkurugenzi wa usalama wa Marekani James Clapper, kitendo cha Urusi kuingilia uchaguzi wa Marekani mwaka uliopita kilikuwa cha ajabu kushuhudia katika utendaji kazi wake.
Akizungumza katika Baraza la senate Nchini Marekani, Clapper amesema udukuzi huo wa barua pepe za chama cha Democratic kuelekea uchaguzi uliofanyika mwezi Novemba ulisimamiwa na Raisi wa Urusi Vladimir Putin, na kuongeza kuwa atatoa taarifa kamili kwa umma wiki ijayo.
Mkurugenzi wa usalama wa Marekani James Clapper
Image captionMkurugenzi wa usalama wa Marekani James Clapper
Clapper amesema kuwa ifikapo ijumaa atatoa mchanganuo wa tafiti zake kwa Rais mteule wa Marekani Donald Trump aliyewahi kulaani na kutilia shaka ushiriki wa Moscow.
Urusi pia imekanusha madai ya kuhusika katika udukuzi huo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*