Marekani kumsaka mtoto wa Osama Bin Laden



Osama Bin Laden alikuwa kiongozi wa Al Qaeda
Image captionOsama Bin Laden alikuwa kiongozi wa Al Qaeda
Marekani imemtaja Hamza ambaye ni mtoto wa kiume wa Osama Bin Laden katika orodha ya Magaidi.
Taarifa kutoka wizara ya ulinzi zinasema Hamza Bin Laden akiwa katika umri wa miaka ishirini amekuwa kiongozi makini wa kundi la Al Qaeda ambao ni wapiganaji wa kundi lililoanzishwa na baba yake.
Taarifa zinasema amekuwa makini katika suala hilo kwa kufuata nyayo za baba yake kwa kujiunga na jihadi na kusambaza ujumbe wa sauti kwa niaba ya kundi la Al Qaeda na kuchochea mashambulizi dhidi ya nchi za Magharibi.
Kwa sasa Atazuiliwa kufanya biashara na wananchi wa Marekani na mali zake zitataifishwa.
Kiongozi mkuu wa usalama wa kundi la Al Qaeda Ibrahim al-Banna ametajwa katika orodha hiyo pia.
Marekani itatoa ofa ya dola Million tano kwa atakayesadia kukamatwa kwa al-Banna.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*