Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete wa tatu kutoka kushoto,akiwa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Singh Bwana Kugis wa pili kutoka kulia,pamoja Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo wa kwanza kushoto baada ya kupokea msaada wa madawati kutoka Jumuiya hiyo.
Mbunge wa Jimbo la Chalinze akipanda mti kuashiria sherehe ya miaka 350 toka kuzaliwa kwa Guru Sing Sikh.
Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo akipanda mti huku Mbunge na Diwani wakishuhudia zoezi hilo
Diwani wa Kata ya Kiwangwa Bwana Malota Hussein akipanda mti kuweka kumbukumbu ya miaka 350 toka kuzaliwa kwa Guru Singh Sikh.
Bwana Makelele, kwa niaba ya wazazi akiwashukuru wahisani hao kwa msaada ya madawati. Aliwashukuru pia kwa kuendelea kusaidia maendeleo ya elimu na huku akiahidi wao wazazi kuunga mkono juhudi hizo
Mwenyekiti wa CCM kata ya kiwangwa akisema neno la kuwashukuru wanajumuiya ya Singh kwa mchango huu ambao yeye amesema kuwa ni juhudi za kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Mwenyekiti wa CCM Dr. John Magufuli. Kwa niaba ya Chama aliwashukuru kwa kuunga mkono utekelezaji wa ilani
Mh.Mbunge akipokea Madawati toka kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Singh.Aliyesimama katikati ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kiwangwa Ndg. Rashid
Mbunge Ridhiwani Kikwete wa tatu toka kulia katika picha ya pamoja na viongozi wa jumuiya ya Sing . Pembeni ya Mbunge upande wa kushoto ni Bwana Kugis ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo na wa kwanza kulia ni katibu wa Jumuiya hiyo
Comments