Wafungwa 55 wapoteza maisha katika vurugu Brazil


  • a
Ulinzi uliimarishwa baada ya tukio hilo
Image captionUlinzi uliimarishwa baada ya tukio hilo
Maafisa nchini Brazil wanasema wafungwa 55 wamepoteza maisha katika vurugu zilizotokea katika gereza nje ya mji wa Manaus.
Vurugu hizo katika gereza la Anisio Jobim zilianza siku ya Jumapili na kuisha baada ya saa kumi na saba pindi wafungwa hao waliposalimu amri.
Baadhi ya miili imekatwa vichwa huku mingine ikiwa imechomwa moto.
Mkuu wa usalama katika jimbo la Amazonas, Sergio Fontes, amewaambia waandishi wa habari kuwa vurugu hizo zilikuwa zimepangwa muda mrefu.
"kila kitu kinaashiria kwamba vurugu zilizotokea zilikuwa zimepangwa muda mrefu.
Idadi kubwa ya wafungwa waliotoroka walikamatwa
Image captionIdadi kubwa ya wafungwa waliotoroka walikamatwa
Wafungwa waliweka bayana kwa uongozi wa gereza kwamba kila kitu kitakuwa sawa katika msimu huu wa sikukuu.
Hawakutekeleza ahadi yao, lakini huwezi kuwaamini wahalifu?"
Fontes ameongeza kusema kuwa baadhi ya wafungwa walitoroka na wengine wameuawa.
Hata hivyo, Idadi kubwa ya wafungwa waliokuwa wametoroka tayari wamekamatwa.
Nako nje ya gereza, ndugu wa wafungwa waliokusanyika walijawa na shauku ya kutaka kujua hali ya ndugu zao.
Mama wa mmoja ambae mwanae ni mfungwa ameonekana akishikilia gamba la risasi huku akisema polisi hawana nia ya kuwalinda wafungwa.
Maafisa wa gereza wanasema makundi hasimu yaliyopo nje na ndani ya gereza yamepigana kwa kutaka kuwa na sauti dhidi ya kundi jingine.
Ndugu na jamaa wakiomboleza nje ya gereza
Image captionNdugu na jamaa wakiomboleza nje ya gereza
Wajumbe wa moja wapo ya makundi hayo, wametengwa katika magereza mengine.
Nae waziri wa katiba amekwenda katika gereza hilo ili kuangalia uwezekano wa kuhamishwa kwa baadhi ya wafungwa katika gereza jengine.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI