Waziri wa Nishati Prof. Muhongo APIGA STOP Bei Mpya za Umeme



WAZIRI mwenye dhamana ya kusimamia Nishati na Madini hapa nchini, Prof. Sospeter Muhongo, leo Desemba 31, 2016 amesimamisha mara bei mpya za manunuzi ya umeme zilizopitishwa na kutangazwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), kuwa bei ya umeme itapanda kwa asilimia 8.5% ifikapo Januari 2017.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Felix Ngamlamgosi jana, ongezeko hilo la bei ni kufuatia maombi ya Shirika la Umeme nchini, (TANESCO), ambalo liliwasilisha maombi EWURA ya kutaka ongezeko la bei kwa asilimia 18.19.

Ewura Kupandisha Bei ya Umeme 8.5% Kuanzia Januari

Taarifa iliyotolewa leo na Waziri Prof. Muhongo imeitaka EWURA kusitisha mara moja utekelezwaji wa mpango huo wa kuongeza asilimia 8.5% ya bei ya umeme, na badala yake isubili maamuzi mengine ya serikali itakapojiridhisha baada ya kupitia ripoti rasmi zote zitakazowasilishwa na EWURA, ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha wadau wote wa masuala ya nishati.
bei-ya-umeme-tanesco

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI