1
Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu ambaye pia ni Mkurugenzi
wa huduma ya Upasuaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Bashir Nyangasa na Dk. Sun Long wakimfunga
bandeji mgonjwa leo mara baada ya
kumaliza kumfanyia upasuaji wa kuunganisha mishipa ya damu (AVF- Arterio Venous
Fistula) kwa ajili ya kusafishia damu kwa wagonjwa wenye matatizo ya figo (Hemodialysis).
Daktari
bingwa wa upasuaji wa kifua, moyo na
mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Wambura Wandwi (Kulia)
na Dkt. Bingwa wa Upasuaji Hussein Hassan wakimfanyia mgonjwa leo upasuaji wa
kuunganisha mishipa ya damu (AVF- Arterio Venous Fistula) kwa ajili ya
kusafishia damu kwa wagonjwa wenye matatizo ya figo (Hemodialysis). Kushoto ni
Afisa Muuguzi wa chumba cha upasuaji Sr. Elina Mulenda.
4
Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu ambaye pia ni Mkurugenzi wa
huduma ya Upasuaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Bashir Nyangasa (aliyevaa kofia ya pinki)
akiwaonyesha kitu Dkt. bingwa wa
upasuaji wa kifua, moyo na mishipa ya damu Wambura Wandwi (Kulia) na Dkt.
Bingwa wa Upasuaji Hussein Hassan wakati wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa
kuunganisha mishipa ya damu (AVF- Arterio Venous Fistula) kwa ajili ya
kusafishia damu kwa wagonjwa wenye matatizo ya figo (Hemodialysis).
Picha
na Anna Nkinda - JKCI
Comments