Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akihojiwa mbele ya kamati ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge mjini Dodoma leo kufuatia mwito wa Kamati hiyo kumtaka afike kujibu tuhuma zinazomkabili za kuingilia haki, uhuru na madaraka ya Bunge kutokana na matashi aliyoyatoa mapema Februari mwaka huu, Dar es Salaam yaliyokuwa na madai ya kudharau Bunge. (PICHA NA BUNGE)
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Paul Makonda akipokelewa katika Viwanja vya Bunge na Mkuu wa Kitengo cha Babari, Elimu na Mawasiliano Ndg. Owen Mwandumbya
Wito wa kufika mbele ya Kamati hiyo unafuatia Azimio la Bunge lilitolewa tarehe 8 Februari 2017 ambapo Bunge liliazimia Mhe. Spika aweze kukubali Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Alexandra Mnyeti na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Mhe Paul Makonda wahojiwe kutokana na Matamshi yao ya Kudharau Bunge.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Paul Makonda akipokelewa katika Viwanja vya Bunge na Mkuu wa Kitengo cha Babari, Elimu na Mawasiliano Ndg. Owen Mwandumbya
Comments