Katibu
Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana, asubuhi hii amemaliza ziara yake
katika
wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma na kuanza safari ya kwenda Kyela mkoani
Mbeya, ambako
ataanza ziara rasmi ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM, kusikiliza
kero za wananchi na kujadiliana nao njia ya kuzipatia ufumbuzi.Pichani,
Kinana na wajumbe wake wa
sekretarieti ya CCM, Nape Nnauye (Itikadi na Uenezi) na Dk. Asha-Rose
Migiro (Siasa na Uhusiano wa Kimataifa), wakiwapungia mikono wananchi
wa Nyasa, baada ya kupanda Mv Songea, kuanza safari ya kwenda Kyela.
Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Ernest Kahindi
Kwaherini wakazi wa wilaya ya Nyasa,sasa tunaelekea wilaya ya kyela mkoani Mbeya.
Baadhi
ya wananchi na wanachama wa CCM wakiwa na shamra shamra wakati
wakiusindiza ujumbe wa Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana walipokuwa
wakielekea Kyela mkoani Mbeya mapema leo asubuhi kuendelea na ziara
yake.
Comments