Katibu Mkuu
wa Chama cha Wafanyakazi wa Uhifadhili Mahotelini na Majumbani kwa Huduma za Jamii
na Ushauri (CHODAWA), Said Wamba akizungumza na waandishi wa habari wakati
kongamano na baadhi ya matawi ya vyama wafanyakazi Dar es Salaam. (PICHA NA
DALILA SHARIF)
Na Dalila Sharif
KATIBU Mkuu wa
Chama cha Wafanyakazi wa Uhifadhili Mahotelini na Majumbani kwa Huduma za Jamii
na Ushauri (CHODAWA), Said Wamba amezitaka
Sekta za wafanyakazi zisizorasmi kujiunga kwa kuanzisha vyama vya wafanyakazi
na taasisi binafsi ili kuweza kulinda na kutetea maslahi yao.
Akizungumza na
waandishi wa habari katika kongamano hilo la matawi ya vyama vya wafanyakazi (CHODAWO),
Jijini Dar es Salaam leo alisema umuhimu wa vyama vya wafanyakazi ni kusaidia
kulinda na kutunza maslahi ya wafanyakazi na wafanyabiashara ndogondogo.
Alisema
wafanyakazi wengi na wafanyabiashara nchini wamekuwa hawajui kusimamia haki zao
na kukabiliana na matatizo yanayowakabili katika shughuli zao za kukuza uchumi
wa Taifa hilo.
“Wafanyakazi na
wafanyabiashara wanatakiwa kuunda vyama kwa lengo la kuweza kuwatatulia
matatizo yanayowakabili wanapokuwepo kazini na kukabiliwa na majanga au kudai
haki ya kazi zake endapo amedhulumiwa , chama kinauwezo mkubwa wa kuwasilisha
changamoto zao,”alisema Wamba.
Mratibu wa
Shirikisho wa (CHODAWA) Vicky Kanyoka alisema kuwa wafanyakazi wanawake wa
majumbani wa haki ya kusimamiwa haki zao katika kuwatetea na kuwasehea hivyo
wapo baadhi ya waafanyabiashara wanawake hufanya kazi na kuanzisha baisahara
bila kuwa na vyama na kushindwa kusimamia haki zao.
“Mifano mizuri
nchini India wanawake wanashirikiana na kuwana muungano wa vyama vya
wafanyakazi katika kutetea na kulinada maslahi yao katika ufanyaji kazi hali
ambayo inawasaidia kuaendaelaea vyaema katika uazlishaji uchumi,”alisema
Kanyoka.
Comments