ACACIA YAONGOZA MAONESHO YA WIKI YA USALAMA NA AFYA KAZINI 2017 MKOANI KILIMANJARO





Maonesho ya wiki ya usalama na afya kazini yameanza leo siku ya Jumatano tarehe 26/04/2017 katika viwanja vya Ushirika mjini Moshi mkoani Kilimanjaro ambapo taasisi mbalimbali za serikali na binafsi zimepata fursa ya kuonyesha namna zinavyozingatia masuala ya usalama na afya kazini kwa wafanyakazi wao. 

Miongoni mwa taasisi zilizopata fursa ya kushiriki maonyesho hayo kwa mwaka huu ni pamoja na kampuni za uchimbaji wa madini za Bulyanhulu, Buzwagi na North Mara ambazo zinamilikiwa na kampuni ya uchimbaji ya Acacia.

Ambapo katika maonesho hayo migodi hiyo ya imekuwa ikionesha vifaa mbalimbali vya uokozi pamoja pamoja na mbinu zitumikazo kuhakikisha mazingira ya usalama kwa wafanyakazi wao wawapo kazini.

Maadhimisho ya mwaka huu ya siku ya afya na usalama mahali pa kazi yameandaliwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) yakiwa na kauli mbiu ya “ Ongeza wigo wa ukusanyaji na utumiaji wa takwimu za usalama na afya” .Maadhimisho hayo yanatarajiwa kufikia kilele chake Aprili 28,2017.

Zifuatazo ni picha mbalimbali wakati wa maonesho hayo siku ya kwanza Aprili 26,2017
Banda la mgodi wa Bulyanhulu-Maafisa kutoka mgodi wa Bulyanhulu wakiandaa kupokea wageni mbalimbali 
Maandalizi yanaendelea
Maafisa kutoka mgodi wa Bulyanhulu 
Msaidizi wa Meneja Mkuu wa mgodi wa Acacia Bulyanhulu Margaret Mandia akimkaribisha Mkaguzi wa Mitambo Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kanda ya Kaskazini Boysafi Sabato katika banda la mgodi wa Bulyanhulu
Mkaguzi wa Mitambo Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kanda ya Kaskazini Boysafi Sabato akifurahia jambo baada ya kufika katika banda la mgodi wa Bulyanhulu
Afisa Mazingira mgodi wa Bulyanhulu Florence Nyuki akimwelezea Mkaguzi wa Mitambo Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kanda ya Kaskazini Boysafi Sabato namna mgodi huo unavyotunza mazingira na kuhakikisha usalama unakuwepo katika maeneo yao ya kazi
Afisa Mazingira mgodi wa Bulyanhulu Florence Nyuki akitoa ufafanuzi kwa mwananchi aliyefika katika banda la mgodi wa Bulyanhulu
Afisa uhakiki wa usalama kutoka mgodi wa Bulyanhulu Amina Mohamed akimwelezea kuhusu masuala ya usalama mgodini kwa mmoja wa wananchi waliofika katika banda hilo
Afisa Mazingira mgodi wa Bulyanhulu Florence Nyuki akitoa maelezo kwa maafisa kutoka shirika la Umeme nchini Tanzania (TANESCO) waliotembelea banda hilo
Wananchi wakiwa katika banda la mgodi wa Bulyanhulu 
Afisa rasilimali watu mgodi wa Bulyanhulu Mwanaisha Mosha akiwaelezea watalii kuhusu DVD ya Bulyanhulu inayohusu usalama mgodini na mahusiano ya jamii 
Afisa viwango vya usalama mgodi wa Bulyanhulu Setieli Kimaro akitoa elimu kuhusu mambo ya usalama mgodini kwa wananchi waliotembelea banda la la mgodi wa Bulyanhulu
Mdau kutoka Mgodi wa Williamson Diamonds Limited Gamba Isack akiangalia bango kubwa lililopo katika banda la mgodi wa Bulyanhulu
Wananchi wakiwa katika banda la mgodi wa Bulyanhulu 
Afisa afya mgodi wa Bulyanhulu Tumaini Sylvanus akielezea kuhusu masuala ya afya mgodini
Afisa Mahusiano mgodi wa Bulyanhulu William Chungu akifurahia jambo na mwananchi aliyembelea banda la mgodi wa Bulyanhulu
Mhandisi wa uchimbaji mgodi wa Bulyanhulu Fikiri Thomas akiwaonesha wananchi namna wanavyochimba madini
Banda la mgodi wa Buzwagi- Maafisa kutoka mgodi wa Buzwagi wakijiandaa kwa ajili ya maonesho
Nje ya banda la mgodi wa Buzwagi
Mkufunzi Idara ya Uokozi mgodi wa Buzwagi Azaeli Kitange akitoa elimu kuhusu usalama mgodini kwa wananchi waliotembelea banda la mgodi wa Buzwagi
Maandalizi yanaendelea
Afisa usalama na afya mgodi wa Buzwagi Mustapha Mlewa akiwaelezea wananchi kuhusu namna mgodi huo unavyojitahidi kuhakikisha wafanyakazi wake wanakuwa salama mgodini
Mwananchi akiuliza swali kwa maafisa kutoka mgodi wa Buzwagi
Mkufunzi Idara ya Uokozi mgodi wa Buzwagi Azaeli Kitange akimwonesha mwananchi aliyetembelea banda la mgodi huo vifaa vinavyotumika katika uokoaji mgodini
Afisa usalama na afya mgodi wa Buzwagi Mustapha Mlewa akitoa somo kwa wananchi waliotembelea banda la mgodi wa Buzwagi
Afisa Usalama na afya mgodi wa Buzwagi Deogratius Nyantabano akimwelezea mwananchi namna mgodi huo unavyojitahidi kuhakikisha wafanyakazi wake wanakuwa salama kazini

Afisa Usalama na afya mgodi wa Buzwagi Deogratius Nyantabano akiendelea kutoa elimu kwa wananchi
Afisa Usalama na afya mgodi wa Buzwagi Deogratius Nyantabano akieleza jambo kwa mwananchi aliyetembelea banda la mgodi wa Buzwagi
Dkt. Ludovick Silima kutoka mgodi wa Buzwagi akitoa elimu ya usalama kwa wananchi waliotembelea banda la mgodi huo
Dkt. Ludovick Silima kutoka mgodi wa Buzwagi akielezea masuala ya afya kwa wananchi waliotembelea banda la mgodi wa Buzwagi 
Wananchi wakiwa katika banda la mgodi wa Buzwagi 
Banda la Mgodi wa North Mara- Maafisa kutoka mgodi wa North Mara wakijiandaa kuanza kufanya maonesho 
Afisa usalama mgodi wa North Mara Samwel Nyansika akimwelezea masuala ya usalama mgodini mwananchi aliyetembelea banda hilo 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.