MBUNGE BOBALI ATOA MSAADA WA VIFAA VYA MICHEZO JIMBONI

Na Mwandishi Wetu
MBUNGE wa Jimbo la Mchinga, mkoa wa Lindi, Hamidu Bobali ametoa vifaa vya michezo kwa timu za Aston Villa ya kata Mchinga Two na Timu ya Waasi FC ya kata ya Milola pamoja na mipira minne ikiwa ni ahadi yake kwa timu hizo.
Bobali alitekeleza ahadi hiyo wakati akiwa kwenye ziara ya kikazi aliyoifanya hivi karibuni kwenye jimbo hilo ambapo alipokea kero na changamoto mbalimbali kutoka kwa wananchi.
Akizungumza baada ya kutoa vifaa hivyo vya michezo Bobali alisema matarajio yake ni kuona soka la Mchinga na Lindi kwa ujumla linakuwa hivyo atahakikisha timu zote zinapata vifaa hivyo.
“Mimi ni mchezaji wa mpira hivyo naamini katika michezo ndio maana nimeamua kutekeleza ahadi yangu ya kuwanunulia vifaa ambavyo waliniomba naamini hawataniangusha,” alisema.

Mbunge huyo alisema ni jukumu la Serikali kuweka mazingira ya viwanja vizuri ili kuhakikisha kuwa vijana hao wanashiriki kwani michezo ni moja ya ajira.

Alisema ataendelea kusaidia timu mbalimbali ambapo kwa sasa ni mmoja wa wafadhili wa ligi ya Kanda ya Kusini ambayo inashirikisha timu za kanda hiyo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA