Newcastle yarejea ligi kuu ya England


NewcastleHaki miliki ya pichaPA
Image captionAyoze Perez mfungaji wa mabao mawili ya Newcastle
Klabu ya Newcastle United msimu ujao watakipiga katika ligi kuu ya England ya baada ya kupanda tena daraja kutoka Championship kwa kuichapa timu ya Preston kwa mabao 4-1.
Mshambuliaji wa Newcaste Ayoze Perez ndie aliyeanza kuiandika timu yake goli la kuongoza katika dakika ya saba ya mchezo,Katika dakika ya kumi na nne Preston wakachomo goli hilo kupitia kwa mshambuliaji wake Jordan Hugill,
Kiungo Christian Atsu akaiongezea Newcastle bao la pili katika dakika ya arobaini na tano ya kipindi cha kwanza, katika dakika ya sitini na tano winga Matt Ritchie akaongeza bao la tatu kwa vijana wa Rafa Benitez kwa mkwaju wa penati.
NewcastleHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionWachezaji wa Newcastle wakishangilia ushindi
Mshambuliaji Ayoze Perez tena akashindilia msumari wa mwisho uliowahakishia Newcastle kurejea tena katika ligi kuu msimu ujao.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA