Meneja
wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), mkoa wa Manyara Eng. Bashiri
Rwesingisa, akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani, wakati alipokuwa akikagua mahali ambapo
litajengwa Daraja la Magara lenye urefu wa Mita 84, Wilayani Babati, mkoani
Manyara, jana.
Naibu
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani, akitoa maelekezo
kwa Mhandisi Christopher Saul (katikati), kutoka Wakala wa Barabara Nchini
(TANROADS), mkoa wa Manyara wakati alipokuwa akikagua mahali ambapo litajengwa
Daraja la Magara lenye urefu wa Mita 84, Wilayani Babati, mkoani humo, jana.
Muonekano
wa Sehemu ambapo Daraja la Magara lenye urefu wa Mita 84 katika barabara ya
Mbuyu wa Mjerumani-Mbulu KM 21 litakapojengwa. Mkataba wa ujenzi wake
unatarajiwa kusainiwa mwezi Juni mwaka huu.
Serikali
imesema ipo katika hatua za mwisho za kumpata mkandarasi atakayejenga Daraja la
Magara lenye urefu wa Mita 84 katika barabara ya Mbuyu wa Mjerumani-Mbulu KM 21
lililopo mkoani Manyara ambapo mkataba huo unatarajiwa kusainiwa mwezi Juni
mwaka huu.
Akizungumza
hayo jana kwa wananchi wa Kijiji cha Mayoka, wilaya ya Babati, mkoani humo,
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani, amewataka
wananchi hao kutoa ushirikiano kwa mkandarasi atakayepatikana ili kurahisisha
mradi huo kukamilika kwa wakati.
"Serikali
inaendelea kukamilisha taratibu zake ili kumpata mkandarasi, sasa ombi langu
kwenu ni kuhakikisha kuwa mnatoa ushirikiano kwa Mkandarasi huyo pindi
atakapofika eneo la kazi", amesema Naibu Waziri.
Amebainisha
kuwa Serikali imekuwa ikitenga fedha mwaka hadi mwaka ili kuweza kukamilisha
mradi huo ambapo kwa mwaka wa fedha 2017/18 zaidi ya Shilingi Bilioni 1
zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa KM 1.2 za barabara sehemu ya mlima Magara
ambayo itajengwa kwa kiwango cha zege.
Naye,
Meneja wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), mkoa wa Manyara Eng. Bashiri
Rwesingisa amemhakikishia Naibu Waziri huyo kumsimamia mkandarasi
atakayepatikana katika ujenzi wa Daraja hilo ili kuondoa kero na adha
wanayopata wakazi wa Babati na maeneo jirani.
Ameongeza
kuwa ujenzi wa Daraja la Magara pia litahusisha ujenzi wa barabara unganishi
zenye urefu wa KM 2 kwa kiwango cha lami na KM 2 kwa kiwango cha Changarawe.
Daraja
la Magara ni moja ya Daraja litakaloleta chachu ya maendeleo kwa wakazi wa
Arusha, Mbulu na Babati kwani ujenzi wake utarahisisha huduma za usafirishaji
na kukuza utalii kwa nchi kupitia Hifadhi ya Mbuga ya Manyara.
Imetolewa
na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano.
Naibu
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani, akizungumza na
wananchi wa Kijiji cha Mayoka kuhusu mkakati wa Serikali katika ujenzi wa
Daraja la Magara wilayani Babati, mkoani Manyara, jana.
Imetolewa
na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano.
Comments