HABARI MPASUKOOOOO. AJALI YA DALADALA NA LORI YASABABISHA VIFO NA MAJERUHI DAR

AJALI ya daladala na Lori imetokea leo asubuhi jijini Dar es Salaam na kusababisha watu kadhaa kupoteza maisha na wengine kujeruhiwa.

Ajali hiyo iliyohusi daladala linalofanya safari za Msasani- Mbagala limegongana na lori la Azania eneo la Mtava, Barabara ya Nyerere.

Kwa mujibu wa mashuhuda ni kwamba daladala lililokuwa linatokea Gongo la Mboto kwenda Msasani liliharibika vibaya upande wa mbele baada ya kuligonga lori lililokuwa linakatiza barabara kutokea upande wa kushoto kuingia kwenda Tazara..

Miili ya waliokufa na majeruhi wa ajali hiyo walikimbizwa Hospitali ya Muhimbili.

Habari zaidi tutaendelea kuwaletea kwa kadri tutakavyokuwa tunazipata

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI