Abraham Ntambara
HOSPITALI
ya Aga Khan ya jijini
Dar es Salaam wameanzisha ushirikiano na Hospitali ya Aly Khani ya Mjini Mumbai
India kwa lengo la kuboresha huduma za afya nchini Tanzania hususani kwenye
upasuaji wa mifupa katika nyonga na magoti.
Hayo yalibainishwa jana jinini Dar es
Salaam na Mkurugenzi Mtendaji Mkuu Aga
Khan, Sisawo Konteh wakati
akizungumza na waandishi wa habari, alisema ushirikiano huo utakuwa wa muda
mrefu.
“Ndugu zetu hawa kutoka Mumbai India
tumekubaliana waje hapa kuangalia namna tunavyotoa huduma mbalimbali, ili tuone
wapi tunaweza kuboresha hususani huduma zinazoweza kufanywa nchini zifanyike,”
alisema Konteh.
Aliongeza kuwa kutokana na
ushirikiano huo utawapa fursa madaktari nchini kuweza kuongeza ujuzi katika
upasuaji kutoka kwa madaktari bingwa wa hosspitali wa Aly Khan kwani uhusiano
huo utakuwa wa muda mrefu.
Muuguzi Mkuu wa Aga Khan Lucy Hwai
alibainisha kuwa wageni hao wamekuja ili kuboresha uhusiano uliopo baina yo
hospitali hizo.
Alieleza kuwa kwa sasa kuna mladi wa ujenzi
unaendelea wa jingo linalogharimu sh. bilioni 1.7 ambapo alifafanua kuwa
litakapokamilika litakuwa na uwezo wa kuchukua vitanda 170.
Alisema kutokana na idadi hiyo watahitaji
kuwa na wataalamu wakuweza wengi ambao wataweza kufanya huduma za matibabu kwa wa gonjwa watakao kuwa
wakiripoti hospitalini hapo kwa ajili ya matibabu.
“Linatarajia kukamiliaka mwakani
kuanzia mwezi wa sita, ndipo ushirikaono utakapotakiwa zaidi na hii itasaidia
sana wagonjwa ambao walitakiwa kupelekwa India wataweza kupatiwa matibabu
nchini,” alisema Hwai.
Hwai alisisitiza kuwa ili kuhakikisha
usharikano huo unaboresha huduma za afya, utaenda sambamba katika kutoa na
kuimarisha elimu kwa madaktari nchini ili watanzania wapate faida katika huduma
za afya.
Aidha alisema kuanzia jana na leo
watatoa huduma ya upasuaji wa nyonga na magoti kwa kushirikiana na madaktari
bingwa kutoka India ambapo alieleza kuwa madaktari hao watakaa watakuwepo hadi
Mei 8 mwaka huu.
Kwa upande wa Mkurugenzi wa hospitali
ya Prince Aly Khan Sanjay Oak, alisema
wameanzisha ushirikiano huo ili kusaidiana kwa pamoja katika kutoa huduma za
upasuaji nchini.
Alisema kwa kipindi sasa hatua katika
huduma za upasuaji zimekuwa zikibadilika kutokana na maendeleo ya teknolojia
ambapo aleleza kuwa yeye amekuwa akifanya huma hiyo kwa zaida ya miaka 30 na
ameshafanya upasuaji kwa watoto zaidi ya 3000.
MWISHO
Comments