ma nilivyokuhaidi, kazi yangu kila Jumapili ni kukuletea nukuu kutoka kwa watu ambao wamefanya mambo makubwa au ya kipekee katika ulimwengu huu. Nukuu za leo zimelenga kukujengea uwezo au kukupa A, B, C kuelekea kwenye mafanikio yako.
- Mtu hubeba mafanikio au kushindwa ndani yake, wala haitegemei na hali ilivyo nje – Ralph Waldo Trime.
- Mafanikio si funguo ya furaha, bali furaha ni funguo ya mafanikio, kama utapenda kile unachofanya utafanikiwa – Albert Schweitzer.
- Ikiwa ndio mara yako ya kwanza kuyafikia mafanikio, bado unatakiwa kufanya kazi kwa bidii kuendelea kusalia hapo –Richard C Miller.
- Weka akilini mwako, kufanikiwa au kushindwa haitoweza kuwa mwisho – Roger W Babson.
- Hakuna siri ya mafanikio bali ni matokeo ya kujiandaa, kufanya kazi kwa bidii na kujifunza kule uliposhindwa – General Colin Powell.
- Kama tuna furaha tumefanikiwa – Anna Kleirmer.
- Kila aliyefanikiwa nyuma yake kuna miaka mingi ya kutokufanikiwa – Bob Brown.
- Mafanikio ni mjumuisho wa jitihada ndogo ambazo hujirudia au kufanyika kila siku – Robert Collier.
Shukrani, dondosha comment yako hapo chini kuelezea ni nukuu ipi imekugusa zaidi.
By Peter Akaro
Comments