KIONGOZI WA ZAMANI WA PANAMA MANUEL NORIEGA AFARIKI


Aliyekuwa Jenerali wa Panama Manuel Noriega yuko katika hali mahututi
Jenerali Manuel Antonio Noriega, kiongozi wa zamani wa kijeshi wa Panama, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 83, maafisa wametangaza.
Noriega alifanyiwa upasuaji hivi majuzi baada ya kuanza kuvuja damu kufuatia upasuaji kwenye ubongo wake.
Noriega awali alikuwa mshirika mkuu wa Marekani lakini aliondolewa madarakani kwa nguvu wanajeshi wa Marekani walipovamia nchi yake mwaka 1989.
Baadaye, alifungwa jela Marekani baada ya kupatikana na makosa ya ulanguzi wa madawa ya kulevya na utakatishaji wa pesa.
Alipatikana pia na makosa Ufaransa, na kisha Panama, ya mauaji, ufisadi na wizi wa mali ya umma.
Alikuwa ameachiliwa huru kutoka gerezani Januari kumruhusu kufanyiwa upasuaji kwenye ubongo wake.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA