Man United kusajili nyota wapya watatu au wanne


UNITEDHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionWachezaji wa United wakishangilia ubingwa wa kombe la Europa ligi
Mabingwa wa taji la Europa ligi msimu huu klabu ya Manchester United inatarajiwa kuweka kikomo cha kufanya usajili kwa wachezaji watatu au wanne muhimu katika dirisha kubwa la usajili
Meneja wa United Jose Mourinho amesema makamu mwenyekiti wa timu hiyo Ed Woodward anajua wachezaji wanaotakiwa kwa zaidi ya miezi miwili iliyopita.
"Ed Woodward anayolisti yangu ya wachezaji ninaowataka ," alisema meneja huyo baada ya mchezo wa Europa ligi dhidi ya Ajax .
Mourinho anataka kuongeza changamoto katika safu ya ulinzi na ushambuliaji ili kuweza kuwania taji la ligi kuu ya England msimu ujao.
UNITEDHaki miliki ya pichaGOOGLE
Image captionAntoine Griezmann moja kati ya nyota wanaowindwa na Man United
United wamekua wakihushwa na kutaka kuimarisha safu ya ushambuliaji kwa kuwasajili Antoine Griezmann toka Atletico Madrid, Andrea Belotti wa Torino pamoja Romelu Lukaku.
Kwa Upande wa safu ya ulinzi wachezaji wanaotajwa kuwa wako kwenye rada ya Mourinho ni beki wao wa zamani Michael Keane anayechezea Burnley,beki kisiki wa Benfica Victor Lindelof na Muholanzi Virgil van. Dijk wa Southampton.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI