Theresia
Maliatabu, mnufaika wa mradi wa Airtel Fursa akimsikiliza mteja wakati
alipohudhuria maonyesho ya bidhaa na kuonyesha kazi ya uchoraji wa picha
za Sanaa anazozifanya hivi
karibuni.
·
Mnufaika wa Airtel FURSA bidhaa zake ziko sokoni mikoa zaidi ya mitano
Mradi
wa Airtel Fursa umeendelea kufanikiwa kwa kuendelea kuwezesha vijana
nchini ambapo mmoja kati ya waliowezeshwa mwaka jana Bi Threria
Maliatabu mkazi wa Mbagala jijini Dar
es Saalam ameelezea jinsi mradi huo ulivyomuwezesha kukuza kipato na
kupata mafanikio ya kuanza kujenga nyumba yake binafsi, kujinunulia
shamba la eka 2 huku akiwaasa vijana wenzake nchni na wale wote
waliowezeshwa na Airtel FURSA kuchangamkia fursa hizi
pindi zinapotokea.
Akiongea
na waandishi wa habari jijini Dar es saalam , Bi Maliatabu ambaye
anajishughulisha na biashara ya uchoraji wa picha za sanaa alisema “
najivunia sana kuwa mmoja kati ya
vijana walioshikwa mkono na Airtel Fursa kwa sababu program hii imeweza
kunitoa kutoka niliopokuwa hadi kufika kwenye haya mafanikio niliyo
nayo leo. Kwakweli nimekuwa na mafanikio makubwa sana ikiwemo kuboresha
kiwango cha bidhaa zangu , nimefanikiwa kuanza
ujenzi wa nyumba yangu ya vyumba vinne na pia nimeweza kukunua shamba
la eka 2 Mkuranga mkoa wa pwani. lengo langu ni kuanzisha shughuli za
kilimo ili kutanua wigo wa biashara yangu lakini pia kuendelea na
shughuli yangu ya uchoraji nayoifanya kwa sasa”
Aidha
Maliatabu alifafanua kuhusu changamoto mbalimbali katika biashara
ikiwemo masoko ya nje , usafiri wa kusambaza bidhaa zake huku akieleza
kuwa baadhi ya changamoto hizi ameshaanza
kuzishughulikia na kuomba wadau mbalimbali kuweza kumsaidia.
“Nimeweza
kuongeza masoko yangu na kufikia masoko ya Zanzibar, Moshi , Arusha na
Dar, na kwa sasa niko katika mchakato wa kupeleka bidhaa zangu nchini
Sweeden na Italy. Mipango hii
ikikamilika kwakweli nitakuwa nimefurahi kufikia malengo yangu na
naamini nitafanya vizuri zaidi na kukuza kipato changu zaidi. Natoa wito
kwa vijana wenzangu kujituma na kufanya kazi kwa bidiii na kutafuta
fursa mbalimbali na kujikita kwenye ujasiriamali
badala ya kusubiri ajira ambazo zimekuwa ni changamoto”.
Akiongea
kuhusu mafanikio haya, Meneja Huduma kwa Jamii, Bi Hawa Bayumi alisema
, tunafarijika na kujisikia fahari kuona jinsi gani program hii imeweza
kuwainua vijana hawa wajasiriamali
wenye nia ya kukuza kipato na kufikia malengo yao. Theresia Maliatabu
ni mfano wa kuigwa, alipowezeshwa alijiongeza na kufanya kazi kwa juhudi
kubwa na maarifa. Nawaasa vijana wajitume na kuchangamkia fursa kama
hizi zinapojitokeza wazitumie vizuri ili kuleta
tija kwenye maisha yao, familia zao na taifa kwa ujumla.”
Theresia
Maliatabu ni moja kati ya vijana waliochagulia kuwa kati ya
wafanyabiashara wadogo wadogo watakaonufaika na mpango wa Airtel FURSA
na kupatiwa vitendea kazi zikiwemo ,
ubao wa kuchorea, vifaa vya kuchorea na computer, mafunzo ya
ujasiriamali na kutengenezewa kipindi maalumu cha Television
kilichoonyesha safari yake katika biashara ambavyo vimemsaidia kukuza
biashara yake. Airtel kupitia mpango wake wa Airtel fursa imewezesha
vijana takibribani 5000 kwa kuwapatia mafunzo ya ujasirimali na baadhi
yao kupata vitendea kazi ili kuboresha biashara zao.
Mwisho
Comments