MSANII UWOYA ATAWAZWA BALOZI WA ITEL TANZANIA

 Meneja wa Bidhaa wa Kampuni ya Itel, Cooper Chen akimtambulisha rasmi msanii maarufu wa  filamu za Tanzania  ‘Bongo Movies’ Irene Uwoya (kushoto) kuwa barozi wa itel Mobile Tanzania kwa muda wa mwaka mmoja katika hafla iliyofanyika Dar es Salaam leo. Kushoto ni Ofisa Habari wa kampuni hiyo, Wolle Fernando na Ofisa Masoko Itel Dar es Salaam, Asha Mzimbili. (NA MPIGAPICHA MAALUMU)
 Wakitiliana saini mkataba

Abraham Ntambara
KAMPUNI ya Itel imemtamburisha rasmi msanii maarufu wa  filamu za Tanzania  ‘Bongo Movies’ Irene Uwoya kuwa barozi wa itel Mobile Tanzania kwa muda wa mwaka mmoja kuanzia jana.
Akizungumza wakati wa jutambulisho huo uliofanyika jana jijini Dar es Salaam Ofisa Habari wa Itel nchini Wolle Fernando, alisema kupitia umaarufu alionao msanii huyo ni imani kwao kuwa ataweza kushiriki nao vyema katika shughuli za kijamii.
“Irene ni msanii maarufu, tunaamini kupitia yeye ataweza kuunganisha itel mobile na watanzania kwa ujumla wao,” alisema Fernando.
Aidha alisema ni matarajio yao kuwa jamii itanufaika kwa kupata elimu kuhusu bidhaa zao kupitia kwake ambapo watasaidiana nae kwenye matukio ya kuonesha ukarimu kwa baadhi ya makundi ya jamii ambayo wanaendesha kupitia charity event programs na mengine.
Alibainisha kuwa wanatambua mchango wa Uwoya katika jamii kwani amekuwa akielimisha kupitia movie zake, hivyo kwa kutambua umuhimu wake watashirikiana kikamilifu kuhakikisha jamii inapata inachotarajia kutoka kwao.
Irine Uwoya alisema atashirikiana na kampuni hiyo vizuri katika shughuli mbalimbali za kijamii ili kuhakikisha jamii inafaidika kupitia charity programs na matukio mengine yanayofanywa itel.
“Nashukuru kwa kupata nafasi hii, nitashirikiana nao vizuri, ntahakikisha kupitia nafasi hii naisaidia jamii yangu ya Tanzania,” alisema Uwoya.

mwisho

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI

KOCHA WA AL.AHLY ASEMA YANGA NI TIMU BORA NA NGUMU